• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Kilimo

Mkoa wa Manyara una eneo la hekta 1,568,117 zinazofaa kwa kilimo ambapo zaidi ya hekta 867,500 zinatumika kwa kilimo cha mazao ya aina mbalimbali. Eneo la kilimo linabadilika kila msimu kulingana na malengo ya wakulima na mwelekeo wa hali ya hewa.

Pia Mkoa una maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji yanayofikia hekta 30,997 na kati ya hizo hekta 11,715 zinatumika kuzalisha mazao ya aina mbalimbali kama vile mahindi, mpunga, miwa, migomba na mazao ya mbogamboga na matunda. Maeneo makubwa yapo Wilaya ya Babati (Bonde la Kiru) na Simanjiro (Ukanda wa Mto Pangani). Maeneo mengine yapo Mbulu (Bonde la Bashay) na Hanang (Bonde la Endagaw na Gocho)

Mazao yanayolimwa ni Mahindi, Alizeti, Mbaazi, Mtama, Ngano, Maharage, Miwa, Vitunguu Maji, Vitunguu Saumu na Mpunga ambayo hutumika kama mazao ya Biashara na Chakula kwa wakazi wa Mkoa. Ziada ya uzalishaji huuzwa kwenye Mikoa mingine na Nchi jirani za Kenya, Somalia, Ethiopia, Eritrea na Sudani.

Moja ya Mashamba ya Mahindi Wilayani Hanang-Mkoa wa Manyara

Moja ya Mashamba ya Mbaazi Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara

Moja ya Mashamba ya alizeti katika Wilaya ya Kiteto Mkoa wa Manyara

Shamba la Ngano katika Wilaya ya Hanang-Mkoa wa Manyara

Mafanikio yaliyopatikana katika Sekta hii yanatokana na jitihada za Serikali na wadau wa maendeleo katika kuimarisha matumizi ya wanyama kazi, matrekta makubwa na madogo (power Tillers), mbegu bora, mbolea na wataalam wa ugani.

Maksai wakitumika kusafirisha mazao shambani

Mwaka 2006, Serikali ilianzisha Mpango wa kilimo wa ASDP kwa lengo la kuongeza uzalishaji mazao kwa kushirikiana na Mradi wa PADEP “Participatory Agriculture Development and Empowerment Project” unaoshirikisha wananchi kuibua Miradi ya Vikundi na Miradi ya Jamii na kuchangia gharama za utekelezaji katika Sekta za Kilimo na Mifugo.

Miundombinu mbalimbali iliweza kujengwa katika maeneo mengi ya Mkoa.

Baadhi ya miundombinu hiyo ni Vituo vya rasilimali za Kilimo na Mifugo, Maghala, majosho, nyumba za maafisa ugani na machinjio.

Aidha, Mkoa unashirikiana na Mashirika na Taasisi za Maendeleo ya kilimo katika kukuza na kuendeleza Sekta ya Kilimo na Mifungo. Mashirika hayo yametajwa katika jedwali lifuatalo na kuonesha majukumu wanayotekeleza.

Mashirika na Taasisi za Maendeleo katika Kilimo

NA
SHIRIKA
MAJUKUMU
ENEO LA UTEKELEZAJI
1.
Farm Africa
Kuimarisha uzalishaji wa Kilimo na Mifugo
Babati, Hanang’ na Mbulu
2.
World Vision
Kuendeleza Sekta za Mifugo, Kilimo.
Simanjiro na Babati
3.
FIDE
Kutoa Mafunzo katika Sekta za Kilimo, hifadhi ya Mazao, Ufugaji, Teknolojia ya biogas.
Babati
4.
TRIAS
Hutoa ufadhili wa fedha kwa Mashirika mengine 13
Babati na Mbulu
5.
FAIDA Mali
Hutoa mafunzona kuwaunganisha wazalishaji na Masoko
Babati na Hanang
6.
SARI
Utafiti katika uzalishaji wa Kilimo na Mifugo.
Wilaya zote za Mkoa
7.
SNV
Kujenga uwezo, Kutoa Ushauri, kuu nganisha wadau mbalimbali wa Maendeleo
Wilaya zote za Mkoa
8.
MVIWATA
Uundaji vikundi vya wakulima, elimu ya Kilimo na Masoko
Wilaya zote
9.
MAI
Kuimarisha Kilimo na Mifugo
Wilaya zote za Mkoa
10
African Rising
Kuimarisha Malisho Bora
Babati
11
COSITA
Kuimarisha Kilimo cha Ufuta
Babati
12
AFAP
Kuboresha kilimo cha maharage na Soya
Babati na Hanang
13
TAHA
Uboreshaji wa Kilimo cha Mbogamboga na Matunda
Babati, Hanang na Mbulu
14
PRISE
Utafiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi
Simanjiro
15
Maisha Bora
Maboresho katika huduma za Mifugo, Maji na Ujasiriamali
Simanjiro
16
MEDA
Uwekaji wa Vitamin A kwenye mafuta
Babati
17
SIDO
Uwezeshaji wa wajasiriamali katika usindikaji mbalimbali na ubunifu
Wilaya zote
18
TPRI
Utafiti na Ushauri katika masuala ya viuatilifu
Wilaya zote

SEKTA YA MIFUGO

Baadhi ya wanyama wafugwao Mkoani Manyara

Mkoa una zaidi ya mifugo milioni 3. Kati ya hao ng’ombe wa asili ni 1,747,683; ng’ombe wa kisasa ni 22,485; Mbuzi wa asili ni 1,411,752; mbuzi wa kisasa ni 27,346; Kondoo wa asili ni 576,889 na wa kisasa ni 10,317; Nguruwe ni 79,696; kuku wa asili ni 1,176,901 na wa kisasa ni 20,813 na punda ni 64,385. Hakika huu ni utajiri mkubwa. Sekta hii pekee imeajiri zaidi ya asilimia 11 ya wakazi wa Mkoa.

Yapo maboresho mbalimbali yaliyofanywa na Serikali kwenye sekta kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo. Maeneo yaliyofanyiwa kazi ni uboreshaji wa kosaafu kwenye kupitia madume bora, ujenzi na ukarabati wa majosho.

Mafanikio ya Sekta ya Mifugo yameongeza uzalishaji wa nyama kutoka kilo 150 hadi kilo 300 kwa ng’ombe mzima na maziwa kutoka wastani wa lita 1 hadi lita 5-10 kwa siku.

Josho lililoko Wilayani Babati Mkoa wa Manyara

Kutokana na Mafanikio hayo, Mkoa una fursa nyingi za kuwekeza katika sekta ya ufugaji hususani uanzishaji wa ranchi na viwanda vidogo vya kusindika mazao ya mifugo kama ngozi, maziwa na nyama. Fursa nyingine ni ujenzi wa majosho na mabwawa. Halmashauri za Mkoa zimetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa aina mbalimbali.

UVUVI

Uvuvi katika Mkoa wa Manyara ni moja ya sekta inayo changia katika kukuza uchumi na kupunguza umasikini kama ilivyo ainishwa katika MKUKUTA.

Mchango wa shughuli za uvuvi katika Mkoa wa Manyara ni mkubwa kwani imetoa ajira kwa watu takribani zaidi ya 1800 wakiwemo wavuvi, wachuuzi wa samaki na wafugaji wa samaki,

Samaki ni chanzo cha protini itokanayo na wanyama, chanzo hiki cha protini ni Muhimu kwani walaji wenye kipato cha chini ambao hawawezi kumudu vyanzo vingine vya protini wanaweza kumudu chanzo hichi kikilinganishwa na vyanzo vingine vya protini itokanayo na wanyama,

Rasilimali za uvuvi katika Mkoa wa Manyara zinapatikana katika maeneo ya wilaya za Babati, Hanang, Mbulu na Simanjiro katika maeneo ya bwawa la nyumba ya mungu, ziwa Babati, ziwa Burunge, Ziwa Manyara na ziwa Bassotu.

Ukuzaji wa viumbe katika maji kwa maana ya ufugaji wa samaki katika mabwawa ya kuchimbwa na yale ya asili ( malambo) pia unafanyika katika Halmashauri zote za mkoa wa Manyara ambapo kuna jumla ya Mabwawa ya samaki yapatayo 121 na malambo 8 yenye samaki.

Baadhi ya zana za uvuvi katika Bwawa la Nyumba ya Mungu

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.