• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

RC Manyara aagiza watumishi wa Idara ya Elimu waliokaa zaidi ya miaka 5 kuhamishwa

Imechapishwa Tarehe: December 16th, 2020

Na: Mariam Juma,Hanang.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Joseph Mkirikiti amemwagiza Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Hanang Solomon Isack  kuwahamisha watumishi wa idara ya elimu wilayani hapo waliodumu kwa zaidi ya miaka 5 kwa kile alichokieleza kuwa hao ndio wanaokwamisha jitihada za ufalu wa watoto wilayani hapo.

Kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa inakuja mara baada ya wilaya hiyo kushika nafasi ya mwisho kimkoa  kwa muda wa miaka mitatu  mfululizo  huku watumishi wa idara hiyo wakishindwa kubuni mbinu mpya za kuongeza ufaulu katika wilaya  

“Nimekuja wilaya hii kama Mkuu wa wilaya hii nikakuta Hanang ni ya mwisho watumishi wa idara hiyo  ni wale wale,mwaka wa pili nikiwa hapa tumefeli kama wilaya tena nikiangalia wataalamu waliopo  bado ni wale wale,mwaka huu tena mmefeli watu ni wale wale nasema  Mkurugezi hamisha watu hawa”alisema  Mkirikiti,

Alisema ili kuhakikisha wanaongeza kiwango cha ufaulu wilayani hapo bila kuwahamisha wataalamu hao wa muda mrefu bado ni tatizo kwani hata wakiwaleta Mafisa elimu wengine wapya bila wataalamu hao wa chini yake kuhamishwa bado itakuwa ni tatizo hivyo kinachotakiwa ni kuwahamisha  na kuleta wengine wapya watakaoisaidia wilaya hiyo  kuongeza ufaulu na kuacha kushika nafasi ya mwisho  Kimkoa kila mara.

Mkirikiti akawataka pia kuhakikisha wanakamilisha miundo mbinu ya madarasa  ili wanafunzi waliofaulu waweze kuingia darasani na kuanza masomo yao.

“Mwanzoni mpaka naondoka hapa tulikuwa na upungufu wa madarasa 78 tukayapunguza yakafika 15 sasa kama yameongezeka nendeni hivyo hivyo  msijipunguzie maana kule mkoani  nikiwaambia nileteeni upungufu wa madarasa mnaniambia hamna upungufu wa madarasa  na mnaupungufu wa madarasa 14 lakini mnatakiwa mjiwekee  lengo la madarasa 30 kwasababu mnasema madarasa yanatosheleza Hanang ni kwasababu mmeendelea kuwa watu wa kufeli,hivyo  kwasababu hakuna wakufaulu madarasa ndio maana yanatosha  na kama wangekuwepo kugekuwa na uhitaji”alsema Mkirikiti.

Pia akamtaka Mkurugenzi  kuwahamisha walimu ambao wamekuwa ni wasemaji wa walimu wenzao na wanaofanya kazi kwa mazoea kwani nao hao ni tatizo na wakwamishaji wa elimu wilayani hapo.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo  Gharibu  Lingo alieleza kuwa jumla ya watoto  wa darasa la saba waliofaulu  kujiunga na kidato cha kwanza ni 4773 na wanaupungufu wa madawati 1837 pamoja na upungufu wa madarasa 30 na yanatakiwa yapatikane ifikapo January 2021.

Mkuu wa wilaya akawataka madiwani wapya walioapishwa kurudi na kujua mikakati ya kumaliza mapungufu  hayo kwa kuwa mikakati ya awali ni kuhakikisha watoto waote waliofaulu  wanaingia madarasani

“Madiwani rudini kwenye  kamati zenu  za maendeleo za kata Ili mkaweke mipango mikakati mtakayokuta wajumbe wenu wameiandaa lakini pia mboreshe na mtakapokwama tuwasiline maana sisi ni wamoja “alisema Lingo.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • Vijana Kiteto wanufaika na Mikopo ya Halmashauri

    January 05, 2021
  • Babati watakiwa kuchangamkia Mikopo ya Serikali

    January 04, 2021
  • Waziri wa Kilimo awataka Wakulima wa ngano kuongeza uzalishaji

    December 24, 2020
  • Njooni muwekeze Manyara- RC Manyara

    December 22, 2020
  • Tazama Zote

Video

Nangwa Sekondari katika muonekano mpya
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2020 Manyara Region . All rights reserved.