• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Huduma za Maji
    • Kitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Procurement
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Huduma ya Maji
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

Wadau Njooni na mpango wa kuendeleza michezo- Naibu Waziri

Imechapishwa Tarehe: April 1st, 2019

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.George Waitara amewataka wadau na wataalamu wa michezo nchini kuja na mpango mahsusi wa namna nchi itakavyoweza kufikia  katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.

Akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kwa ajili ya Mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) kilichoandaliwa na kampuni ya vinywaji ya Coca cola, Mheshimiwa Waitara amesema anatamani kuona walimu na wadau wengine waje na mpango mahsusi wa kuendeleza michezo ili Tanzania iondokane na tabia ya kuwa kichwa cha mwendawazimu katika sekta hiyo.

Mhe.Waitara amesema wataalamu waje na hoja ya kuendeleza sekta na michezo na anaamini kuwa walimu katika hili wana mchango mkubwa katika kuendeleza sekta ya michezo.

Amesema kwa kuwa watanzania wanapenda sana michezo, hakuna sababu ya kuwasononesha na badala yake akataka wataalam wa michezo kuja na mpango kabambe wa kukwamua sekta hiyo.

Mhe.waitara amesema pamoja na mchango mkubwa unaofanywa na walimu nchini katika kuinua maendeleo ya elimu nchini ambapo kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kiwango cha ufaulu kimekuwa kikiongezeka, bado anaamini walimu wana jukumu kubwa katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanafundishwa michezo kwa nadharia na vitendo.

“ Natoa maelekezo kwa walimu wote kuhakikisha kuwa somo la michezo linafundishwa kwa nadharia na vitendo kama mtaala wa elimu unavyoelekeza,” amesema na kuongeza:

“ viwanja vya michezo vifufuliwe na vifanye kazi kama ilivyokusudiwa, viwanja vilivyovamiwa vipimwe na kuwekewa mipaka,” amesema.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya michezo ya umiseta na udhamini kutoka kampuni ya Coca cola, Naibu Waziri ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kudhamini mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika kitaifa mkoani Mtwara kuanzia mwezi juni mwaka huu.

Pia Mhe.Waitara ameipongeza coca cola kwa kuanzisha shindano maalum la kutafuta shule bora zinazoongoza kwa kutunza na kuhifadhi mazingira ambapo mtoto ambaye atafanikiwa kuokota chupa kilo 600 na kuendelea watapata zawadi mbalimbali zikiwemo laptop.

Naibu Waziri amewataka Coca cola kuhakikisha kuwa shindano hilo linazifikia shule nyingi iwezekanavyo na ikibidi lifanyike kwa mikoa yote 26 nchini.

Mhe.Waitara amewaagiza Maafisa Elimu wa Mikoa, na Maafisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazotolewa na kampuni hiyo zinagawiwa kwa walimu watakaoshinda na wanafunzi pia.

Wakati huo huo Naibu Waziri Waitara amewataka Maafisa elimu nchini kuhakikisha kuwa wanawasimamia walimu na wanafunzi ili waweze kupanda miti ya kutosha nchini ili waweze kukabiliana na athari za jangwa.

“Tukitaka kusaidia kampeni ya usafi wa mazingira hatuna budi kuanza na walimu na wanafunzi, tuhakikishe kila mwalimu shuleni anapanda mti mmoja na kila mwanafunzi anapanda miti miwili mmoja nyumbani na mwingine shuleni,” amesema.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Julius Nestory ameipongeza kampuni ya vinywaji ya Coca cola kwa kuendelea kudhamini mashindano ya UMISSETA ambapo mwaka huu kampuni hiyo imeongeza kipengele cha usafi wa mazingira.

Amewataka maafisa elimu kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazonunuliwa na wadhamini coca cola zinawafikia walengwa na kwamba zawadi na jezi hizo kamwe zisiishie mitaani kwa wasiohusika.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2019 July 11, 2019
  • HOTUBA YA WAZIRI MKUU KWA MAAFISA HABARI MWANZA March 19, 2019
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • EWURA YAJA NA VITUO VYA MAFUTA VINAVYOTEMBEA NCHINI.

    November 29, 2019
  • EWURA yawataka wadau wa Mafuta MANYARA Kuepuka kuuza Mafuta Kiholela

    November 29, 2019
  • KAMATI ZA RUFAA ZA UCHAGUZI FANYENI KAZI KWA HAKI- WAZIRI TAMISEMI

    November 06, 2019
  • NANE- NANE KANDA YA KASKAZINI YAFANA

    August 06, 2019
  • Tazama Zote

Video

MNYETI AITAKA HALMASHAURI YA BABATI MJI KUBUNI VYANZO VYA MAPATO
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Singida Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 310-Babati

    Simu ya mezani: 027-2510060 ,027-251

    Simu ya kiganjani: 027-2510066

    Barua pepe: ras@manyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki zote zimehifadhiwa @2017 Mkoa wa Manyara