• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Bilioni 9.88 kukamilisha ujenzi wa Barabara ya Dareda Center – Dareda Mission

Imechapishwa Tarehe: April 8th, 2024

Na Nyeneu, P. R - Dareda

Waziri wa ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa amemuagiza mtendaji mkuu wa wakala wa Barabara kuu nchini (TANROADS) kuhakikisha hawawafumbii macho wakandarasi wanaoshindwa kufanya kazi kwa wakati wanazopewa na serikali na kukwamisha mipango ya serikali ya kuhakikisha kila mkoa unakuwa na barabara zenye viwango.

Bashungwa ameyasema hayo leo katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Barabara ya Dareda – Dongobesh (Kilomita 60) sehemu ya Dareda Center - Dareda Mission yenye urefu wa kilomita 7. Amesema ujenzi huo ni utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wananchi wa mkoa Manyara wa kukarabati barabara korofi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amesema hafla hii ilipangwa kufanyika Disemba mwaka 2023 na iliahirishwa kutokana na maafa yaliyotokana na maporomoko ya matope yaliyotokea Wilayani Hanang ambapo amemshukuru Mhe. Waziri Bashungwa yeye na timu yake kwa kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na maporomoko hayo.

Pia Mhe. Sendiga amesema Barabara hiyo inaunganisha Wilaya mbili ambazo ni Wilaya ya Mbulu na Wilaya ya Babati ambapo ameitaka mamlaka husika kuhakikisha wakati ujenzi unaendelea wananchi wa maeneo hayo wawe wanufaika wa mradi huo kwa kupata ajira ndogondogo wakiwemo mama ntilie kwa ajili ya kuwapikia chakula wakandarasi.

Nae mtendaji mkuu wa TANROADS nchini Mohamed Besta amesema mradi huo utaghalimu kiasi cha shilingi bilioni 9.88 ambapo amemuagiza mkandarasi anaesimamia mradi huo kufanya kazi kwa weledi na kukamilisha kwa muda uliopangwa.

Aidha, Mbunge wa jimbo la Babati Vijijini ambae pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. Daniel Sirro amesema ni kwa muda mrefu wananchi wa Dareda wamekuwa wakilalamikia barabara hiyo, hivyo ujenzi wa barabara hiyo utasaidia kuuunganisha mawasiliano katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa manyara na kukuza uchumi kwa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.