• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

CHANELI YA UTALII KUVUTIA WATALII WENGI TANZANIA

Imechapishwa Tarehe: January 2nd, 2019

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli mpya ya utalii inatarajiwa kuvutia watalii wengi zaidi kuja nchini sambamba na kuongeza pato la taifa.

Akizungumza tarehe 15 Disemba  jijini Dar es salaam, alipokuwa akizindua chaneli hiyo ya utalii inayojulikana kama “Tanzania Safari channel” Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli hiyo mpya itatoa fursa ya kutangaza wanyama mbalimbali waliopo katika hifadhi za wanyama, utamaduni wa watanzania pamoja na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini ili kuvutia watu wengi zaidi kuja kufanya utalii na hatimaye kuongeza kiasi cha fedha kitachochangia katika pato la taifa.

“Chaneli hii ni njia muhimu ya kutangaza utalii ndani na nje ya nchi yetu, ambapo itaongeza idadi ya watu watakaotembelea Tanzania” alisema Waziri Mkuu Majaliwa

Waziri Mkuu Majaliwa aliongeza kuwa kwa sasa watalii wanaokuja nchini kwa mwaka ni milioni 1.3 , na matarajio ya Serikali ni kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia milioni 2 ifikapo mwaka 2020, hivyo chaneli hiyo ya utalii itasaidia katika kufikia lengo hilo la Serikali.

Naye, Waziri Utalii na Maliasili Dkt. Khamis Kigwangala alisema kuwa sekta ya utalii nchini inachangia asilimia 17.7 katika pato la taifa, na katika mwaka 2017 shilingi trilioni 5.04 zilipatikana kupitia sekta hiyo, na hivyo Serikali imeanza kutekeleza mikakati mbalimbali itakayo saidia kukuza utalii na kuongeza pato la taifa

Akitolea mfano  mikakati hiyo kuwa ni “kuimarisha masoko ambapo wataalamu wa utalii wameshafanya maonesho ya barabarani katika baadhi ya nchi na hivi karibuni watafanya maonesho hayo nchini China ili  kuongeza masoko mapya” alisema Waziri Kigwangala

Waziri huyo wa Maliasili na Utalii, alifafanua mikakati mingine ya wizara hiyo ni kuweka mabango yenye picha mbalimbali za vivutio vya utalii  katika barabara inayoelekea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Aidha, Waziri huyo ametoa fursa kwa wasanii mbalimbali wakiwemo wa filamu na  muziki kutumia sehemu za vivutio vya utalii nchini kwa ajili ya kutengeneza kazi zao za sanaa.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, kutoka Zanzibar,  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Saleh Yusuph Mnemo alisema kuwa chaneli hiyo inatarajiwa kuwasaidia watu wengi kufahamu vivutio vya utali vilivyopo nchini sambamba na kuongeza mapato, ambapo Zanzibar peke yake ina vivutio vya mambo ya kale 39.

Naibu Katibu Mkuu huyo, alifafanua kuwa asilimia 80 ya fedha za kigeni zinazopatikana Zanzibar zinatokana na sekta hiyo, huku ikichangia  asilimia 20 katika pato lake la taifa.

 Chaneli hiyo ya utalii inayojulikana kama Tanzania Safari Channel inaonekana kupitia kisimbuzi cha Startimes namba 331, na kurusha matangazo yake kwa lugha mbalimbali

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • RC Manyara amaliza Mgogoro wa ardhi baina ya mwekezaji na wananchi

    September 01, 2021
  • Mkirikiti amkabidhi Makongoro Ofisi rasmi

    May 25, 2021
  • Karibu Manyara Mhe. Makongoro Nyerere!!!

    May 22, 2021
  • Tuweke uzalendo ktk kusajili watoto chini ya miaka mitano - RC Manyara

    April 20, 2021
  • Tazama Zote

Video

Asilimia mbili ya mikopo kwa walemavu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2021 Manyara Region . All rights reserved.