• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2019 YATANGAZWA RASMI LEO

Imechapishwa Tarehe: July 11th, 2019

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) nchini Tanzania leo Alhamisi Julai 11, 2019 limetangaza matokeo ya kidato cha sita ya mwaka 2019


 Katika matokeo hayo yaliyotangazwa na Katibu Mtendaji wa Necta mjini Unguja Zanzibar, Dk Charles Msonde amesema ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 97.58 mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 98.32 mwaka 2019 ikiwa ni sawa na asilimia 0.74.

 Dk Msonde amesema mtihani huo uliofanyika kati ya Mei 6 hadi 23 mwaka 2019, watahiniwa 91,298 walisajiliwa wakiwamo wasichana 37,948 sawa na asilimia 41.56 na wavulana 53,350 sawa na asilimia 58.44.


 Amesema kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 80,216 na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa ni 11, 082.


 Katibu mtendaji huyo amesema kati ya watahiniwa 91,298 waliosajiliwa kufanya mtihani , watahiniwa 90,001 sawa na asilimia 98.58 walifanya mtihani na watahiniwa 1,297 sawa na asilimia 1.42 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za ugonjwa na utoro.


 Dk Msonde amesema watahiniwa wa shule, kati ya watahiniwa 80,216 waliosajiliwa, watahiniwa 79,770 sawa na asilimia 99,44 walifanya mtihani ambapo wasichana walikuwa 33,883 sawa na asilimia 99.57 na wavulana 45,887 sawa asilimia 99.35. Watahiniwa 446 sawa na asilimia 0.56 hawakufanya mtihani.


 Amesema watahiniwa wa kujitegemea kati ya11,082 waliosajiliwa, 10,231 sawa na asilimia 92.32 walifanya mtihani na watahiniwa 851 sawa na asilimia 7.68 hawakufanya.


 “Jumla ya watahiniwa 88,069 sawa na asilimia 98.32 ya watahiniwa waliofanya mtihani wamefaulu,” amesema Msonde


 Watahiniwa Kumi bora Kitaifa kwa masomo ya Sayansi kuanzia namba moja hadi kumi ni


 1. Faith Nicholous Matee (St. Marry’s Mazinde Juu-PCB)

 2. Herman Pauline Kamugisha (Kisimiri-PCM)

 3. Levina Calist Chami (St. Marry Goretti-PCM)

 4. Benius Eustace (Mzumbe-PCB)

 5. Augostino Issaya Omari (Ilboru-PCB)

 6. Satrumin Arbogast Shirima (Temeke-PCB)

 7. Khalid Hussein Abdallah (Feza Boys-PCM)

 8. Assad Y. Msangi (Feza Boys-PCM)

 9. Peter Jovenal Riima (Kibaha-PCM)

 10. Augustine J. Kamba (Feza Boys-PCM)


 Wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri kwa masomo ya Lugha na Sanaa ni

 1. Victor G. Mtui (Feza Boys-EGM)

 2. Paula Nelson Lujwangana (St. Marry’s Mazinde Juu-HKL)

 3. Blandina Kessy Nyage (St.Marry’s Mazinde Juu-HGL)

 4. Eva J. Shitindi (Machame Girls-HKL)

 5. Ruhinda Benedicto Machimu (Geita Adventist-HKL)

 6. Anita Zacharia Massawe (St.Marry Mazinde Juu-HKL)

 7. Karimu Kassimu Muhibu (Nyangao-HKL)

 8. Anold Andrea Msuya (Manyara-HKL)

 9. Latifa Mohamed Mrosso (Ahmes-HKL)

 10. Eliibariki Desidery Baliyanga (Lukole-HKL)


 Waliofanya vizuri Kitaifa kwa masomo ya Biashara ni


 1. Astone Stevin Ngaeje (Kibaha-ECA)

 2. Gift M. Mwakikusi (Tusiime-ECA)

 3. Emmanuel P. Chila (Alpha-ECA)

 4. Athumani Magadula William (Umbwe-ECA)

 5. Stephano Y. Dismas (Kibaha-ECA)

 6. Robert John Tano (Scolastika-ECA)

 7. Shabani H. Shabani (Kibaha-ECA)

 8. Dotee A. Zuberi (Galonos-ECA)

 9. Ernest P. Game (Kibaha-ECA)

 10. Deogratias Ladislaus Msilinga (Kibaha-ECA)


 Katika matokeo hayo Shule Kumi bora zilizoongoza Kitaifa ni


 1. Kisimiri (Arusha)

 2. Feza Boys (Dar es Salaam)

 3. Ahmes (Pwani)

 4. Mwandet (Arusha)

 5. Tabora Boys (Tabora)

 6. Kibaha (Pwani)

 7. Feza Girls (Dar es Salaam)

 8. St. Marry’s Mazinde Juu (Tanga)

 9. Canossa (Dar es Salaam)

 10. Kemebos (Kagera)


 Shule Kumi zilizofanya vibaya Kitaifa ni


 1. Nyamunga (Mara)

 2. Haile Salassie (Mjini Magharibi)

 3. Tumekuja (Mjini Magharibi)

 4. Bumaangi (Mara)

 5. Butuli (Mara)

 6. Mpendae (Mjini Magharibi)

 7. Eckernford (Tanga)

 8. Msimbo (Katavi)

 9. Mondo (Dodoma)

 10. Kiembe Samaki A (Mjini Magharibi)

Kuangali matokeo yote kwa kila shule angalia sehemu ya Matangazo  kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa "MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2019".

Imeandikwa Na: Haji Msovu (Afisa Habari Mkoa)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • Miaka Miwili ya Rais Samia Manyara ni Shangwe tupu Miradi ya Maendeleo

    March 18, 2023
  • SERIKALI YATOA MAAGIZO MGOGORO WA ARDHI KIRU

    February 13, 2023
  • MITI MILIONI 10.5 KUPANDWA MANYARA

    January 27, 2023
  • RC MAKONGORO AMESEMA WALIOCHAGULIWA WATAINGIA DARASANI BILA USUMBUFU WOWOTE

    January 23, 2023
  • Tazama Zote

Video

Karibu Mwenge wa Uhuru 2022 Mkoa wa Manyara
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.