• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

NAIBU WAZIRI OLE NASHA ATOA AGIZO KUHUSU WANAFUNZI WANAOMALIZA DARASA LA SABA

Imechapishwa Tarehe: October 9th, 2018


Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amewataka viongozi  katika ngazi ya  mkoa hadi vijiji kote nchini  kuhakikisha wanafunzi  wanaomaliza darasa la saba hawaondoki katika maeneo yao  kwenda kufanya kazi za ndani wakati wakisubiri matokeo ya kuhitimu darasa la saba kwani kwa kufanya hivyo  kunawaondolea fursa yao ya kuendelea na masomo pindi wanapofaulu.  

Naibu waziri Ole Nasha ametoa agizo hilo mkoani Manyara wakati akizungumza na viongozi hao kuhusu hali ya Elimu mkoani humo ambapo amewataka kusimamia kwa ukaribu suala hilo ili kutokatisha ndoto za watoto hao na kwamba wale wanaofanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

"Hakikisheni watoto hawa wanaposubiri matokeo hawasafirishwi kwani wanapofika huko wanarubuniwa na waajiri hivyo hata matokeo yakitoka na kuonesha wamefaulu hawarejei kuendelea na masomo." Alisisitiza Naibu waziri Ole Nasha

 Amesema fursa za Elimu katika nchi yetu ni kubwa kwa sasa kwa kuwa Elimu msingi ni bure hivyo hakuna kisingizio tena kuwa mtoto hawezi kusoma kwa kuwa mzazi hana fedha

"wazazi msiwe sehemu ya kuchangia watoto wenu kwenda mjini kwa kuwa tu wanawatumia fedha kwa ajili ya matuzi bali hakikisheni mnawasimamia watoto hao katika kipindi chote wanachosubiri matokeo na kuwapeleka shule pindi matokeo yanapotoka na kuonekana wamefaulu,"aliongeza Naibu waziri Ole Nasha

Amewataka viongozi hao kutumia sheria kuhakikisha watoto wenye umri wa kuandikishwa wanaandikishwa  ili kutokuwa na wimbi kubwa la watoto wa mitaani wasioenda shule.

Awali Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara Arnold Msuya alimweleza Naibu waziri wa Elimu kuwa mkoa huo una mwamko mdogo wa Elimu  hasa katika jamii ya wafugaji hali   inayopekea kutowaandikisha shule watoto wao wenye umri wa kuanza shule.

Naibu waziri Ole Nasha pia ametembelea  Chuo cha Ufundi stadi VETA Manyara na kuwataka kupitia mitaala yao ili iendane na wakati, ikidhi mahitaji ya soko lakini pia wanafunzi weweze kusoma vitu vingi kwa wakati mmoja na viwe ni vile vinavyoendana  na soko la ajira ili kuongeza fursa ya vijana kujiajiri pindi wanapomaliza masomo yao.

(Kwa Picha mbalimbli na Video za matukio angalia Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha na Maktaba ya Video)

Imeandikwa Na: Haji Athumani (Afisa Habari Mkoa wa Manyara)

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • RC Manyara amaliza Mgogoro wa ardhi baina ya mwekezaji na wananchi

    September 01, 2021
  • Mkirikiti amkabidhi Makongoro Ofisi rasmi

    May 25, 2021
  • Karibu Manyara Mhe. Makongoro Nyerere!!!

    May 22, 2021
  • Tuweke uzalendo ktk kusajili watoto chini ya miaka mitano - RC Manyara

    April 20, 2021
  • Tazama Zote

Video

Asilimia mbili ya mikopo kwa walemavu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2021 Manyara Region . All rights reserved.