• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

NAIBU WAZIRI WA MAJI ASISITIZA USHIRIKIANO KATI YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

Imechapishwa Tarehe: February 11th, 2026

Na, Ruth Kyelula, Manyara RS

Naibu Waziri, Wizara ya Maji, Eng. Mathew Kundo (MB) amesisitiza juu ya ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuboresha huduma za maji na usafi wa mazingira Mkoani Manyara, hasa Wilayani Hanang' ambapo miradi mingi ya maji inatekelezwa.

Aliyasema hayo Februari 11, 2026, wakati akizindua Mpango wenye gharama za uwekezaji wa huduma za maji, usafi wa mazingira na usafi binafsi (WASH), ambapo umezinduliwa Wilayani Hanang', Mkoani Manyara.

Aidha amesema kuwa, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo  na sekta binafsi, imepiga hatua kubwa katika kuboresha huduma za maji  na usafi wa mazingira katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni.

"Huu ni utekelezaji kwa vitendo wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia maboresho yaliyofanyika katika sera ya Taifa ya maji na ya mwaka 2002 Toleo jipya la mwaka 2025 ambapo imesisitiza mashirikiano ya Serikali na sekta binafsi katika kuboresha huduma za maji safi na usafi wa mazingira." Alisema Eng. Kundo.

Naibu Waziri, aliendelea kusema kuwa, Mpango wenye gharama za uwekezaji wa maji, usafi wa mazingira na usafi binafsi (WASH) wa miaka miaka mitano (2026 - 2030) unaolenga kupanua huduma za maji, kuboresha miundombinu ya usafi wa mazingira na kuimarisha usimamizi wa WASH katika jamii Wilayani Hanang' unalenga kuongeza upatikanaji wa maji safi hadi angalau asilimia 95 na kuhakikisha shule zote na vituo vya kutolea huduma za afya vinakuwa na huduma za msingi za WASH, hatua ambayo itakayochangia kuboresha afya na ustawi wa wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa Hanang', Asia Halamga, amewashukuru Water Aid Tanzania, kwa kazi kubwa wanayoifanya katika Wilaya yao,  na pia amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumfikishia kila mwananchi maji ndani ya nyumba yake.

Nae Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Almishi Hazali, aliwapongeza Water Aid Tanzania kwa kuleta miradi ya maji Hanang' na kusema kuwa Wilaya ina Kata 33 na mpaka sasa ni vijiji 20 tu ndio vilivyokosa maji na amemuomba Naibu Waziri awasaidie kuongea na TANESCO pamoja na RUWASA waungane ili kuweza kumtua mama ndoo kichwani kwa asilimia mia moja.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • NAIBU WAZIRI WA MAJI ASISITIZA USHIRIKIANO KATI YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    February 11, 2026
  • NAIBU WAZIRI WA AFYA AAGIZA MIRADI ILIYOFIKIA ASILIMIA 96 NA 94 IMALIZIKE NA KUANZA KAZI MARA MOJA

    November 26, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MANYARA AKABIDHIWA MAJIKO BANIFU 7,914 KWA BEI YA RUZUKU

    November 10, 2025
  • WAKURUGENZI WA HALMASHAURI ZA MKOA WA MANYARA WATAKIWA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA MIKATABA YA LISHE.

    September 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.