• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Rais wa T.F.F – Tutafanya jambo kwa ajili ya Mpira Manyara

Imechapishwa Tarehe: September 1st, 2020

Imeandikwa Na: Haji Msovu (Afisa Habari - Mkoa wa Manyara)

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (T.F.F) Wallace Karia ameahidi kuleta mabadiliko katika soka Mkoa wa Manyara kwa kuboresha miundo mbinu ya viwanja ili kuhakikisha mechi kubwa za kitaifa zinachezwa katika Mkoa huo.

Akizungumza na waandishi wa Habari jana Mjini Babati, Rais Karia ameitaka Halmashauri ya Mji wa Babati ambao ni wamiliki wa Uwanja wa Kwaraa kuhakikisha uwanjwa huo unazungushiwa majukwaa ili Shirikisho litume wataalamu kwa ajili ya kushughulikia eneo la kuchezea.

Rais huyo amesema kwa sasa shirikisho hilo linapita kwenye mikoa ambayo ipo chini kisoka ili kuangalia uwezekano wa kuinua soka katika mikoa hiyo.

“Kuna Mikoa ambayo ipo chini Kisoka ikiwemo Mkoa wa Manyara ambapo timu ya Morani ambayo ilikuwa chini ya mikono yangu tangu ishuke daraja haijawahi kutokea timu nyingine kubwa Zaidi” Alieleza Karia


Karia amesema Uongozi wa mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na TFF watahakikisha mkoa huo unakuwa na viwanja ambavyo vitawezesha timu kubwa kufika katika mkoa huo na kusaidia kuongeza pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

Karia amesema ana imani kubwa na mkuu wa mkoa Joseph Mkirikiti kwa kuwa alishaonyesha nia ya kuendeleza michezo na miundombinu ya viwanja wakati alipokuwa Mkuu wa wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi huku akiisaidia Majimaji ya Songea kupanda daraja.

Kwa upande mwingine Rais Karia amesisitiza kufanyika kwa program mbalimbali katika shule za Msingi na Sekondari ili kukuza soka la vijana na wanawake na kwamba wapo tayari kuleta walimu wa soka katika shule ambazo hazina walimu Pamoja na kutoa mafunzo kwa walimu wa Michezo waliopo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Joseph Mkirikiti amewataka wafanyabiashara wote waliopewa maeneo kuzunguka Uwanja wa Kwaraa kukamilisha haraka ujenzi wa vibanda ili kuzipata fursa zilizoahidiwa na TFF.

Ikumbukwe kuwa safari ya Rais wa TFF Bwana Wallace Karia katika uongozi wa Soka ilianzia Mkoani Manyara alipokuwa Mtumishi wa Umma katika Wilaya ya Kiteto kama Mweka Hazina.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.