• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Watanzania watakiwa kujiunga na CHF iliyoboreshwa

Imechapishwa Tarehe: December 15th, 2020

Mkurugenzi wa Huduma za afya, lishe na ustawi wa jamii Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt Ntuli Kapologwe amewataka waganga wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa.

Dkt. Kopologwe ametoa wito huo jana wakati akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake juu ya uhamasishaji wa jamii kujiunga na mfuko wa bima ya afya ilioboreshwa (CHF) ili kupunguza gharama zisizo za lazima wakati wa kupata huduma za afya kwa wananchi.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo Dkt. Kapologwe ameeleza kuwa asilimia 86 ya wananchi hawajajiunga na Bima ya afya nchini kutokana na kutopata elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kuwa na bima ya afya ya jamii.

“Umuhimu wa kujiunga na bima ya afya ya jamii ni kuepuka gharama za matibabu za hapo kwa hapo katika hospitali,vituo vya Afya na zahanati zetu zilizopo nchini.

Pia amesema kuwa faida ya CHF iliyoboreshwa ni kuwa imeongeza wigo mpana wa upatikanaji wa huduma kwani ukiwa na hiyo bima popote pale ulipo nchini unaweza kupatiwa huduma za afya tofauti na awali huduma ilikuwa katika eneo ulilojiandikisha.

Hivyo taratibu za kujiunga na bima hiyo mwananchi anakwenda kujiandikisha katika ofisi za mitaa, vijiji, vitongoji na mawakala walio katika maeneo yao ili kuweza kusaidia wananchi kujiunga bila vikwazo.

“Baada ya maboresho kuna mfumo ambao unawezesha kutambua mtu wapi alisajiliwa na wapi ametibiwa na kurahisisha urejeshaji wa fedha katika kituo cha kutolea huduma husika”, ameeleza Mkurugenzi huyo.

Vile vile amesema kuwa bima ya afya iliyoboreshwa imepanua wigo wa mafao kwa kuongeza baadhi ya huduma kupatikana katika bima hiyo kama upasuaji mkubwa na mdogo.

Hivyo takribani vituo 6,000 vinauwezo wa kuwahudumia wananchi wanaojiunga na CHF iliyoboreshwa ikiwemo Zahanati 4,922, Vituo vya Afya 716, Hospitali za Wilaya 179 na Hospitali za Mikoa 28.

Aidha Dr. Ntuli aliongeza kuwa kwa upande wa ada kulifanyika utafiti kuweza kujua ni kiasi gani mwananchi anaweza kumudu ili aweze kuchangia ambapo asilimia 98 walisema wana uwezo wa kuchangia shilingi 30,000 ambapo ndicho kiasi kinachotumiwa kwa kila kaya moja ya watu wapatao sita kwa mwaka mmoja.

“Ada hiyo ni kwa maeneo yote isipokuwa Mkoa wa Dar es Salaam ambao ada yao ni shilingi laki moja na nusu kwa kaya moja yenye idadi ya watu sita na shilingi elfu arobaini kwa mtu mmoja na hii ni kutokana na wigo wa vituo vya kutolea huduma katika Mkoa huo ambapo vituo binafsi vitashirikishwa katika utoaji wa huduma ”,amesisitiza .

Pia amesema kuwa mwananchi akiwa amechangia kiasi hicho kwa mwaka na Serikali inachangia kiasi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa mwananchi.

Dkt.Kapologwe ameeleza kuwa tayari Serikali imechangia ruzuku ili kuhakikisha inaboresha huduma za mfuko wa bima ya afya ya jamii.

Mchango wa Serikali katika kuboresha huduma za afya imeboresha miundombinu kwa kujenga hospitali za wilaya mpya 102, vituo vya afya 487, zahanati 1198, ununuzi wa vifaa tiba kwa lengo la kuhakikisha huduma bora zinatolewa ili kutimiza matakwa ya wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.