• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

Imechapishwa Tarehe: December 13th, 2022


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Angellah J. Kairuki amewataka Viongozi wa Sekretarieti za Mikoa, Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na wajumbe wa timu za utekelezaji wa mradi wa BOOST kuhakikisha wanasimamia kwa ufanisi utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa elimu ya Awali na Msingi ili kufikia malengo ya serikali ya kutatua changamoto za elimu nchini.

Mhe. Kairuki ameyasema hayo leo Disemba 13, 2022 wakati akifungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo Makatibu Tawala wa Mikoa, Maafisa Elimu wa Mikoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na wajumbe wa timu za utekelezaji wa mradi wa BOOST katika Mikoa ya Singida, Manyara na Arusha, uliofanyika Jijini Arusha.

Serikali inapimwa kwa vigezo katika kutekeleza Mradi wa BOOST nchini, sitakuwa tayari kuona fedha zimetolewa kiasi cha shilingi trilioni 1.15 na kupelekwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa lakini miradi haitekelezwi kwa wakati na fedha hizo kurudishwa, tutakuwa hatujatenda haki kwa wananchi” amesisitiza Waziri Kairuki

Waziri Kairuki amewataka Wajumbe wa mradi huo kuhakikisha fedha zinazotolewa katika utekelezaji wa miradi zinakamilisha miradi iliyopangwa ili kuepusha miradi mingi kutokukamilika huku fedha zikiwa zimekwisha. Vilevile amewataka wajumbe hao kuhakikisha wanaimarisha ushirikiano na jamii katika utekelezaji wa mradi, pia kuzingatia sheria, kanuni na miongozo katika utekelezaji wa mradi ili thamani ya fedha iliyotolewa iendane na majengo yatakayojengwa ili kufikia matokeo yaliyokubalika.

Aidha, amewaagiza Wajumbe hao kuwahamasisha wazazi/walezi kuwapeleka watoto wenye umri wa kuanza shule ili waandikishwe na kuanza shule kwa wakati ili kuwaepushia mzigo walimu kwa kulazimika kurudia kufundisha mambo yale yale kutokana na wanafunzi wengine kucheleweshwa kuanza shule.

Mhe. Waziri Kairuki amesema katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itatoa shilingi bilioni 240 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi, hivyo amewaagiza kusimamia ujenzi huo ili ukamilike kwa wakati kwa kuzingatia miongozo na wajiepushe na migogoro ambayo huchangia kuchelewesha utekelezaji wa miradi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.