• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

Halmashauri hakikisheni Kidato cha Kwanza wote wanaenda shule 2021 -Katibu Tawala Manyara.

Imechapishwa Tarehe: December 18th, 2020

 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara Bwana Musa Missaile ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa huo kuhakikisha wanajenga madarasa pamoja na kutengeneza madawati ili wanafunzi wote 557 waliokosa nafasi za kujiunga kidato cha kwanza 2021 katika shule za sekondari zilizopo mkoani Manyara wawe wamesharipoti shule ifikapo mwezi Februari 2021.

Katibu Tawala ameyasema hayo leo alipokuwa katika kikao cha uchaguzi wa wanafunzi  wanaotakiwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2021 kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara.

“Halmashauri hizi ambazo watoto wamekosa nafasi zihakikishe madara na na madawati yake yamekamilika ili watoto waingie madarasani !!” Alisema Katibu Tawala.

Akielezea mbele ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho Kaimu Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Elimu Bwana Lago Sillo alisema kuwa kati ya watahiniwa 31981(Wavulana 15,143 na Wasichana 16,838) walioanza darasa la kwanza mwaka 2014, watahiniwa 30800 (Wavulana 14426 na wasichana 16,374) walifanya mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi na watahiniwa 1181 (Wavulana 717 na wasichana 464) hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro,vifo, ugonjwa  n.k

Vilevile Bwana Sillo amesema kuwa watahiniwa wamefaulu Zaidi katika Somo la Kiswahili na Somo la Kiingereza ndo somo lililokuwa la mwisho.

Bwana Lago Sillo pia aliwataja wanafunzi kumi bora wasichana na wavulana waliofanya vizuri ikiwa na Pamoja na shule na Halmashauri walizotoka.

Wanafunzi kumi bora Wasichana katika Mkoa wa Manyara

Na
Jina la Mwanafunzi
Shule anayotoka
Halmashauri
1
Glory Samweli Mathiya
Deira
Babati Mji
2
Laura Leonce Gwandu
Deira
Babati Mji
3
Joyce Jackson Fissoo
Mount Hanang
Hanang
4
Lilian Deogratias Lyakinana
Deira
Babati Mji
5
Doreen Agustino Darema
Laalakir
Kiteto
6
Joyce Paschali Sulumo
Laalakir
Kiteto
7
Monica Emanuel Muhandi
Amka Afrika
Babati Mji
8
Ester Albert Ngara
St.Clare
Babati Mji
9
Judith John Butta
Deira
Babati Mji
10
Monica Kimirei Masiaya
Laalakir
Kiteto

Wanafunzi kumi bora Wavulana katika Mkoa wa Manyara

Na
Jina la Mwanafunzi
Shule anayotoka
Halmashauri
1
Deusdedith Korduni Lengaram
Blue Tanzanite
Simanjiro
2
Elihuruma Samson Thomas
Mount Hanang
Hanang
3
Ibrahim Moses Mollel
New Light
Simanjiro
4
Celvin Leonard Sulley
Mount Hanang
Hanang
5
Jovin Emanuel Kirenga
Blue Tanzanite
Simanjiro
6
Mudathir Izadin Ramadhani
Blue Tanzanite
Simanjiro
7
Bosco Thomas Mollel
Deira
Babati Mji
8
Elia Cosmas Kessy
Amka Afrika
Babati Mji
9
Beatus Sekey Ayo
Laalakir
Kiteto
10
Eliseus Amnaay Sarwat
Laalakir
Kiteto

Shule kumi zilizofanya vizuri Kimkoa

Na
Shule
Halmashauri
1
Laalakir
Kiteto
2
Kazamoyo
Simanjiro
3
Deira
Babati Mji
4
New Vision
Simanjiro
5
Barazani
Mbulu Wilaya
6
Kweli L. Centre
Hanang
7
St.Clare
Babati Mji
8
Aldersgate
Babati Mji
9
Mount Hanang
Hanang
10
New Light
Simanjiro

Akielezea jinsi Halmashauri zilivyofaulisha katika Mkoa wa Manyara Bwana Lago Sillo alisema kuwa Halmashauri ya Mji wa Babati imeshika nafasi ya kwanza kwa kupata asilimia 84.33 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji wa Mbulu iliyopata asilimia 81.47 na ya tatu ni Halmshauri ya wilaya ya Babati iliyopata asilimia 74.5 huku Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ikiwa ya mwisho kwa kupata asilimia 67.43 ikifuatiwa na Halmashuari ya Wilaya ya Mbulu asilimia 68.92 na Kiteto asilimia 71.74.

Angalia majina ya Kila Mwanafunzi na shule aliyochaguliwa kwenye sehemu ya Matangazo

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • RC Manyara amaliza Mgogoro wa ardhi baina ya mwekezaji na wananchi

    September 01, 2021
  • Mkirikiti amkabidhi Makongoro Ofisi rasmi

    May 25, 2021
  • Karibu Manyara Mhe. Makongoro Nyerere!!!

    May 22, 2021
  • Tuweke uzalendo ktk kusajili watoto chini ya miaka mitano - RC Manyara

    April 20, 2021
  • Tazama Zote

Video

Asilimia mbili ya mikopo kwa walemavu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2021 Manyara Region . All rights reserved.