• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

KATAZO LA MIFUKO YA PLASTIKI NI FURSA YA KUANZISHA VIWANDA

Imechapishwa Tarehe: May 16th, 2019

WAKUU wa Mikoa kote nchini wametakiwa kutumia fursa ya tamko la Serikali la kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki kwa kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya mifuko rafiki wa mazingira.

Pia wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kutekeleza agenda ya serikali ya kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa jana jijini hapa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo na kusema ni vyema wakuu wa mikoa wakamasisha ujenzi wa viwanda vya mifuko mbadala ambavyo vitasaidia upatikanaji wa bidhaa hiyo na kutoa ajira katika maeneo yao

“Sasa mifuko ya plastiki haitatumika tena, pia kuna fursa  ya ujenzi wa viwanda, jambo hili litupe nafasi sisi wakuu wa mikoa kama mifuko ya plastiki haitumiki tuangalie jinsi gani katika kampeni yetu ya ujenzi wa viwanda vidogo, kati na vikubwa tukatumia fursa hii.

Aliongeza: “Mnakumbuka katika kampeni yetu ya miezi 12 ya kila mkoa kujenga viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vipatavyo 100, lengu letu ilikuwa vijengwe viwanda 2,600 lakini tukajikuta viwanda 4,887 vimejengwa, kilikuwa ni kiwango kikubwa sana, hivyo sasa mtumie katazo la serikali kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya mifuko rafiki wa mazingi, mrangi mmoja ukigungwa fursa maeneo mengi ya viwanda katika meneo yenu.

Aidha, Jafo pia amewataka wakuu wa mikoa kuhakikisha wanasimamia ipasavyo katazo la mifuko ya platiki katika maeneo yao ili kuiwezesha Tanzania kuungana na nchi zilizokataa kutubia bidhaa hiyo.

“Ikiwa Juni 1 mwaka huu itakuwa mwanzo wa kutotumia mifuko ya plastiki, wakuu wa mikoa mnadhamana, tukiamua kukomesha hili kwa kuhakikisha mnaunga mkono agenda ya serikali ya kupiga matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo imekuwa na madhara ya kiafya na kimazingira.

“ Wakuu wa mikoa mlifanya kazi nzuri sana pale serikali ilipopiga marufuku matumizi ya pombe za viroba, na sasa hali ni nzuri na huwezi kuioana mahali, basi ni imani yangu hata hili la marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki mkisimama kidete litafanyika,” alisema.

Mwezi uliopita, Serikali ilitoa Tamko la kusitisha matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini ifikapo Juni Mosi 2019, katazo lililolenga kuepusha athari za kiafya na mazingira zinazoendelea kujitokeza kutokana na matumizi ya mifuko hiyo.

Katazo hilo lililotolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa linahusu kupiga marufuku uzalishaji, uingizaji, usafirishaji nje ya nchi, usambazaji, uuzaji na matumizi ya mifuko ya plastiki ya aina zote.

Katika kukabilana na hilo, Serikali imejipanga kuendesha operationi kabambe nchi nzima ya kusakama bidhaa hiyo.

Msako huo utahusisha vyombo vya ulinzi na usalama, kamati za ulinzi na usalama za mikoa, wilaya, mamlaka za serikali za mitaa, Maabara ya Mkemia Mkuu wa serikali, Shirika la Viwango Tanzania(TBS), Mamlaka ya Chakula na dawa(TFDA) Ofisi ya Taifa ya Mashitaka na Viwanja vya Ndege, Bandari, Forodha, Uhamiaji na Usafiri wa Nchi Kavu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.