• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Mhe. Rais azikumbusha Halmashauri zote nchini na wananchi kupanda miti

Imechapishwa Tarehe: October 14th, 2023

Na Mwandishi wetu - Mjini Babati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amehitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Mkoani Manyara na kuhudhuria Misa Takatifu ya kumuombea Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Kanisa la Parokia ya Roho Mtakatifu lilipo Mjini Babati. 

Pia Mhe. Rais amesisitiza kuziishi falsafa za Mwalimu Nyerere na kutozipuuza ikiwa ni pamoja na kudumisha Umoja ambayo ni moja ya falsafa ambazo Mwalimu Nyerere alihimiza katika maisha ya uhai wake. Ameongeza kuwa Serikali imeweka jitihada za kuboresha maisha ikiwemo ujenzi wa Vyuo ya VETA ambapo lengo ni kuwajengea Vijana hao ujuzi.

Vilevile Mhe. Rais amezikumbusha Halmashauri zote nchini na wananchi kupanda miti na kutochoma moto ovyo mashamba, kwani kufanya hivyo kuna sababisha mabadiliko ya tabia ya nchi. Pia, amezipongeza Taasisi zinazofanya kampeni juu ya upandaji miti na utunzaji wa mazingira. Mhe. Rais amesisitiza mashindano juu ya upandaji miti yaendelee ili kuhamasisha zoezi la upandaji miti na kutunza mazingira.

Mhe. Dk.Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi kuwashauri wananchi kuacha kilimo cha zao la bangi na kulima mazao ya biashara au kufanya shughuli zingine za kiuchumi tofauti na hizo za madawa ya kulevya kwani hakina tija na kinaleta madhara kwa Taifa. Sambamba na hilo amewataka wananchi kuchukua tahadhari kubwa juu ya ugonjwa wa Ukimwi, amesisitiza kuhusu umuhimu wa lishe huku akiwataka Wakuu wa Mikoa kulishughulikia suala hilo ili kupunguza na kuondoa changamoto ya udumavu.

Mwenge wa Uhuru 2023 wenye kaulimbiu “Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Viumbe hai na Uchumi wa Taifa” umekimbizwa katika Mikoa 31 na Halmashauri 195 za Tanzania Bara na Visiwani kuhamasisha Amani, Umoja, Upendo na Mshikamano wa Kitaifa, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo ambapo Mwenge ulipita na kuwahimiza Wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Picha na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.