• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Mhe. Sendiga atoa shukrani kwa Wananchi wa Mkoa wa Manyara

Imechapishwa Tarehe: October 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amezishukuru Taasisi zilizopo Mkoa wa Manyara, Kamati za maandalizi, Waratibu wa mbio za mwenge wa uhuru 2023, Waandishi wa Habari na wananchi wote wa mkoa wa Manyara kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha katika maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023. Akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake mapema leo, Mhe. Mkuu wa Mkoa pia, amevipongeza vyombo vya ulinzi na Usalama kwa kuweka mazingira ya Usalama kwa muda wote mkoani humo.

Maadhimisho ya kilele cha mbio za mwenge wa uhuru 2023 yaliambatana na ibada ya kitaifa ya kumbukizi ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Kanisa la Parokia ya Roho Mtakatifu lililopo Mjini Babati na maadhimisho ya wiki ya vijana kitafa 2023 yaliyofanyika katika uwanja wa stendi ya zamani Babati Mjini.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho ya kibiashara ambayo yanafanyika Mjini Babati kuanzia tarehe 17 hadi tarehe 21 mwezi Oktoba 2023. Mhe. Sendiga amewataka wafanyabiashara kutumia maonesho hayo kutangaza biashara zao na kutangaza vivutio vya utalii pamoja na fursa za uwekezaji zilizpo Mkoani humo.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amelezea kuhusu Kampeni ya “Mama Samia nivishe viatu”, hii ni kampeni inayolenga kuwavisha viatu watoto wanaoishi mazingira magumu ambapo kwa sasa kampeni hiyo ipo mkoani Manyara na mpaka kufikia leo tarehe 17 Oktoba, 2023 kampeni hii imefanikiwa kuwavisha viatu watoto wasiopungua Elfu moja (1,000) kutoka katika shule Nne za wilaya ya Hanang’ na Wilaya ya Babati.

Mama Samia nivishe Viatu ni kampeni inayoongozwa na Msanii Steve Mengele maarufu kama Steve Nyerere, Msanii Yvonne Cherrie maarufu kama Monalisa, na wasanii wengine waliongozana nao. Kampeni hii kwa mkoa wa Manyara imelenga kuwavisha viatu watoto zaidi ya 2000 ambapo jumla ya pea 2800 za viatu zitatolewa ikiwa ni kwa lengo la kuhakikisha wanafunzi wanaotokea katika mazingira magumu wanapata viatu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.