• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Miaka 59 ya Muungano Umoja na Mshikamano ndio Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu

Imechapishwa Tarehe: April 26th, 2023

Na Nyeneu, P. R -  Gallapo

Kufuatia maelekezo ya serikali kuwa maadhimisho ya sherehe za Muungano kwa mwaka huu zifanyike katika ngazi ya Mikoa nchini kote, Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Charles Makongoro Nyerere leo tarehe 26 Aprili, 2023 ameungana na wananchi wa Mkoa huo kuadhimisha kilele cha sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika Katika Kijiji cha Gallapo Wilayani Babati ambapo kauli mbiu ni “Umoja na Mshikamano ndio Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu”.

Maadhimisho haya ambayo yameanza kufanyika kuanzia tarehe 17 Aprili, 2023 yaliambatana na shughuli mbalimbali za kijamii hususan upandaji miti, usafi wa mazingira na mashindano ya michezo na sanaa mbalimbali. Kadhalika, yaliambatana na Mashindano ya uandishi wa Insha kwa shule za Msingi na Sekondari na washindi washindi wa katika mashindano mbalimbali wamezawadiwa vyeti na fedha taslimu.

“Lengo kuu la Muungano huu ilikua ni kuendelea kudumisha uhusiano baina ya pande hizi mbili ambao umekuwepo kwa muda mrefu katika nyanja mbalimbali kama vile undugu wa damu, biashara, utamaduni, lugha na mahusiano ya karibu ya kisiasa baina ya vyama vya TANU na ASP ambavyo baadae viliunda Chama Cha Mapinduzi”. Alielezea Mhe. RC.

Vilevile Mhe. Makongoro amewapongeza sana wananchi wa Mkoa wa Manyara kwa kuuenzi Muungano kwa vitendo kwa kuimarisha Mshikamano, Ulinzi na Usalama unaowezesha watu wote kufanya kazi za uzalishaji mali kwa amani na utulivu na hivyo kukuza uchumi wa Mkoa na Nchi kwa ujumla.

Lakini pia amewapongeza kwa kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza miradi ya maendeleo ambapo hadi sasa Mkoa umefanikiwa kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kama vile Kuongeza idadi ya Shule za Msingi na Sekondari ambapo hadi sasa Mkoa una jumla ya Shule za Msingi 642 na Sekondari 154, Kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za Afya mwaka hadi mwaka ambapo hadi sasa Mkoa una jumla ya Zahanati 186, Vituo vya Afya 29, na Hospital 12; Aidha, hali ya upatikanaji wa dawa muhimu imefikia 91%

Pia, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mahiri ambapo ameendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.