• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

MKOA WA MANYARA WABORESHA HUDUMA ZA AFYA

Imechapishwa Tarehe: August 28th, 2018

Wadau wa Afya wa mkoa wa Manyara wamekutana tareha 27 na 28 mwezi wa 8 mwaka 2018 katika Halmashauri ya wilaya ya Hanang kujadili taarifa mbalimbali za kiafya ,changamoto,mafanikio, malengo ya kuboresha afya na kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za kiafya.

Akifungua kikao hicho Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mh. Joseph Mkirikiti alisema alitoa shukrani kwa wadau wote walioshiriki, taasisi na mashirika binafsi na amefurahishwa na jinsi ambavyo idara ya afya na vituo vyake jinsi ilivyopanga mikakati ya kimaendeleo na malengo mahususi ya kuboresha afya katika mkoa wetu ili hali tunapitia changamoto mbalimbali lakini anatumai ushirikiano wetu na umoja wetu baina ya serikali, mashirika na wadau tunaweza kufikia lengo na kuboresha huduma za afya kwa wananchi kwa wakati alisisitiza”

Akisoma taarifa ya mradi wa shirika la msaada la Watu wa Marekani (USAID) BORESHA  AFYA  meneja wa kanda ya Kaskazini Dkt. Leo Haule amesema kuwa serikali ya Mkoa wa Manyara kwa ushirikiano wa mradi wa USAID BORESHA AFYA  wamefanikiwa kupiga hatua katika huduma za upimaji wa VVU, kutoa dawa za ARV na dawa za kufubaza makali ya virusi vya ukimwi zinapatikana na kuwafikia wananchi kwa wakati.

Aidha alisema kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita kati ya mwezi april 2017 hadi juni 2018 kwa ufadhili uliotolewa na shirika la msaada la kimarekani (USAID)  ambapo jumla ya wananchi 184,802 walipatiwa huduma za upimaji pamoja na ushauri nasaha katika vituo vinavyofikiwa na mtu mmojamoja.  Kati ya hao jumla ya wananchi 3,114 walipatikana na maambukizi ya VVU ambao ni sawa na asilimia1.7 halikadhalika wananchi 2050 walianzishiwa dawa za kufubaza makali ya VVU ambao ni sawa na asilimia 66 ya wananchi wote waliokutwa na maambukizi.

Pia kwa kipindi cha toka April 2017 hadi jun2018 jumla ya wananchi 2243 walipimwa uwingi wa VVU katika damu,katiyao 1850 ambao ni sawa na asilimia 82 walikutwa na virusi vilivyofubaa. Vilevile tangu july 2017  hadi june 2018 USAID BORESHA AFYA na kamati za afya za Halmashauri zote saba na kamati za afya za mkoa zimewezesha asilimia 90 ya wananchi wote wanapata huduma za tiba na matunzo kufanyiwa uchunguzi wa kifua kikuu, ambapo jumla ya wagonjwa 2,948 wa kifua kuu waliweza kuibuliwa na kupatiwa matibabu, kati ya hao 360 walipatikana na maambukizi ya VVU ambao ni sawa na asilimia12 .Pia jumla ya wananchi 315 walikutwa na kifua kikuu na VVU kwa pamoja na kuanzishiwa dawa za kufubaza makali ya VVU ambao ni sawa na asilimia 88.

Vilevile idadi ya wajawazito wapatao 31,431 walipimwa VVU na kati ya 326 walikutwa na maambukizi ikiwa ni sawa na asilimia moja ,katiyao 305 walianzishiwa dawa ya kufubaza makali ya VVU  ambao ni sawa na asilimia 94 ya wajawazito wote waliokutwa na maambukizi. Shirika la Elizabeth Glaser linalopambana na VVU/UKIMWI kwa watoto (EGPAF) kwa ushirikiano na serikali na Engender health linatekeleza mradi wa USAID BORESHA AFYA katika mikoa sita ya kati na kaskazini mwa Tanzania ukiwamo Manyara.

USAID BORESHA AFYA unatekeleza afua zinazochangia juhudi za serikali kutokomeza maambukizi mapya ya VVU ifikapo mwaka 2030.Hili linafanyika kwa kuweka juhudi kufikia malengo ya kitaifa ya 90, 90, 90 yaani kupima asilimia 90 ya watu wote ili wajue hali zao,kuanzishiwa dawa za kufubaza makali ya VVU asilimia 90 ya waliokutwa na maambukizi ya VVU na kuhakikisha asilimia 90 ya wanaotumia dawa wanakuwa na virusi vilivyofubazwa.

Hadi sasa  USAID BORESHA AFYA inatekeleza afua za upimaji na matibabu kwenye vituo vya tiba 38 katika Halmashauri saba za mkoa wa Manyara ambapo katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 Halmashauri hizo zilipatiwa jumla ya Tsh billion 1 na million 150 ili kutekeleza za afua za upimaji na matibabu ya VVU/UKIMWI,uzazi wa mpango na kifua kikuu.

Pamoja na uzinduzi huo kutakuwa na kampeni ya upimaji virusi vya ukimwi siku ya tarehe 29 katika viwanja vya shule ya Msingi Katesh wilaya ya Hanang ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni” furahayangu,pima,jitambue,ishi”

Kwa Picha na Video mbalimbali angalia Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha 

Imeandikwa Na: Isabela Joseph (UDSM- Mafunzo kwa Vitendo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.