• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Mkurungenzi Malinga atekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Manyara

Imechapishwa Tarehe: April 1st, 2020

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati Bwana Hamisi Malinga akiambatana na Maafisa Afya wa Halmashauri hiyo jana Machi 31,2020 wametekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Alexander Mnyeti alilolitoa siku ya Jumatatu Machi 30 alipotembelea Kiwanda cha kutengeneza vitakasa mikono kilichopo Babati Mjini na kuzitaka Mamlaka zote za Serikali za Mitaa zilizopo katika Mkoa wa Manyara kuhakikisha Vitakasa mikono vinasambazwa katika maeneo yote na hasa kwenye mikusanyiko ya watu.

Mkurugenzi Malinga na timu yake alitekeleza agizo hilo kwa  kutembelea Mnada wa Dareda/ Ayalagaya na kutoa elimu juu ya kujinga na Ugonjwa wa Corona kwa wafanyabiashara na wateja katika maeneo ya Minada.

Mkurugenzi Malinga aliwaambia wafanyabiashara hao kuhakikisha wanachukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa maji yanayotiririka, kuacha kusalimiana kwa kushikana mikono, kuziba mdomo kwa maungio ya mkono wakati wa kupiga chafya na kutumia vitakatisha mikono ili kujikinga na ugonjwa huo kwani kinga ni bora kuliko tiba.

“Ndugu wafanya biashara na wateja wa eneo hili hakikisheni mnachukua hatua zote zinatotakiwa kuchukuliwa ili kujinga na janga hili la Corona” Alisema Mkurugenzi huyo.

Kuhusu Malalamiko ya vitakasa mikono kupanda bei Mkurugenzi huyo  aliwahakikishia Wananchi kuwa Serikali ya Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na kiwanda cha kutengeneza vitakasa mikono cha Mati Super Brands kilichopo Babati Mjini itahakikisha bidhaa hizo zinapatikana kwa wingi na kwa bei nafuu katika maeneo yote ya minada na katika makazi ya watu pia.

“Kamati ya usalama ya Mkoa wa Manyara na Wilaya ya Babati tukiongozwa na Mkuu wetu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Alexander Mnyeti ilitembelea kiwanda cha kutengeneza vitakatisha mikono kilichopo Babati na watuhakikishia bidhaa hizo zimezalishwa za kutosha na zitauzwa kwa bei ambayo kila mwananchi atamudu kuinunua” Aliongeza Mkurugenzi Malinga.

Akizungumza katika mnada huo Meneja masoko wa kiwanda hicho Bwana Mvungi alisema kuwa wametengeneza vitakasa mikono kwa kila ujazo na bei tofauti kulingana na kipato cha Mtanzania wa kawaida.Bei ya kiwandani ya bidhaa hizo ni kuanzia shilingi 1500 hadi 125000 kutegemeana na ujazo.

Kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi Afisa Afya wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Bwana Suten Mwabulango aliwaambia wafanyabiashara mnadani hapo watumie elimu watakayoipata kuwafikishia ujumbe wengine kwenye minada mbalimbali na hata Nyumbani kwao kwa familia zao kwani jukumu la kuelimisha ni la kila mmoja wetu.

“Nawashauri ndugu zangu hakikisheni mnaitumia elimu mtakayoipata hapa kuwafikishia na wengine kwenye minada mnapozunguka na hata majumbani kwenu” Alisisitiza Afisa Afya huyo.

Akiongea kwa niaba ya Wafanyabiashara wa Minada wote Mwenyekiti wa Minada  Bwana Khalifa Ally aliwataka wafanyabiashara wenzake kufuata ushauri unaotolewa na wataalamu ili kujikinga na maradhi hayo na kuwahakikishia wataalamu hao kuwa wamejitahidi kuweka ndoo za kunawia mikono kila mahali pamoja na kuweka Jeshi la akiba ili kuwalazimisha wananchi kunawa mikono waingiapo na kutoka mnadani.

Elimu ya kujikinga na mlipuko wa Corona katika Mkoa wa Manyara inaendelea kutolewa kila sehemu ili kujikinga na ugonjwa huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.