• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Mkuu wa Mkoa wa Manyara azindua usajili wa vizazi na vifo kwa njia ya Kielektroniki

Imechapishwa Tarehe: August 24th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Joseph Joseph Mkirikiti amewataka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi hasa wanaoishi mbali na mijini juu ya Huduma ya Usajili wa Vizazi na Vifo kwa njia ya Kielektroniki (E-HUDUMA) ili huduma hiyo iwafikie wananchi wengi iwezekanavyo na kuondoa usumbufu kwa kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo.

Mheshimiwa Mkirikiti ameyasema hayo leo Agusti 24, 2020 alipokuwa akizindua mafunzo ya huduma ya usajili wa vizazi na vifo kwa njia ya Kielektroniki kwa Wakurugenzi wa Halmashauri,Maafisa Taarafa,Maafisa Elimu wa Halmashauri na Maafisa Elimu kata katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Babati Mkoani Manyara.

“ Nitumie nafasi hii kuwataka RITA mfike maeneo yote kutoa elimu juu ya kutumia huduma hii ili tuweze kuwapunguzia wananchi usumbufu na gharama kwa kusafiri umbali mrefu kufuata vyeti katika Ofisi za RITA ambazo mara nyingi zinakuwa katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya”Alisema Mhe.Mkirikiti.

Huduma hizo za usajili wa vizazi na Vifo kwa njia ya Kielektroniki zinamwezesha Mwananchi kutumia simu za kisasa popote alipo kufanya maombi ya vyeti vya kuzaliwa,kuhakiki cheti cha kuzaliwa au kifo, kutuma,kutuma maombi mapya ya vyeti vya kuzaliwa au vifo na kuhakiki cheti cha kuzaliwa au kifo kwa urahisi.

Ili kupata huduma hiyo tembelea tovuti ya RITA www.rita.go.tz kisha bonyeza kitufe kilichoandikwa “E- HUDUMA”, Fungua akaunti ya usajili itakayokuwezesha kutuma na kufuatilia mrejesho wa maombi yako halafu Chagua huduma unayoihitaji na fuata muongozo/maelekezo yaliyotolewa.

Mfumo huu utatoa fursa kwa wananchi wengi kupata cheti cha kuzaliwa akiwa nje ya eneo (Wilaya) alipozaliwa au tukio la kifo lilipotokea.

Wakati huohuo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara amefanya Kikao na Wafanyabiashara wa Mkoa huo na kuwataka kutafuta fursa zilizomo Mkoani Manyara ili kuwekeza na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Mkoa hu.

Aliyasema hayo leo alipokuwa akiongea na makundi mbalimbali ya wafaanyabiashara wa Mkoa wa Manyara baada ya kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara Mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa amewataka Wafanyabiashara hao kujenga mahusiano mazuri na Serikali yao na kuhakikisha wanazitambua fursa zilizopo na kuzifanyia kazi.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.