• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Mnyeti ataka vitakasa mikono kusambazwa kila kona Manyara

Imechapishwa Tarehe: March 31st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Alexander Mnyeti amewataka wakazi wa mkoa huo kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na  Serikali  na wataalamu wa Afya ili kujikinga  na maambukizi ya ugonjwa wa Corona unaoambukiza na kuua kwa kasi Duniani.

Aidha amewaonya wafanyabiashara wanaouza vitakasa mikono (Sanitizer) wenye tabia ya kubadilisha bidhaa husika  na kupoteza ubora uliopo  na wanaouza kwa bei ya juu tofauti na maelekezo ya Serikali na kwamba watakaobainika kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Mhe.Mnyeti amezungumza hayo siku ya Jumatatu Machi 30  alipotembelea kiwanda cha Mati Super Brands Ltd cha mjini Babati ambacho kimeamua kushirikiana na Serikali kutengeneza vitakasa mikono ili kupambana na virusi vya Corona na kuviuza kwa bei elekezi ya serikali.

“Tujitahidi sana kujikinga, hicho ndo sisi tunaweza kwani tukisubiri ugonjwa  uingie,usambae halafu ndo tutafute matibabu itatusumbua sana, kwa hiyo tujitahidi sana kwenye kujikinga kabla ugonjwa haujasambaa” Alisisitiza Mnyeti.

Katika ziara yake kiwandani  hapo Mkuu wa Mkoa ameupongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kujali afya za wananchi huku akiwataka waendelee kuzalisha kwa wingi bidhaa hizo ili wananchi wa Mkoa wa Manyara na Mikoa ya jirani waweze kuzipata kwa urahisi. Pia ameutaka uongozi wa kiwanda hicho kuhakikisha bidhaa hiyo inazalishwa kwa wingi na kusambazwa katika maeneo yote ndani na nje ya Mkoa yenye uhitaji.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara  Bwana Missaile Musa ameeleza kuwa bidhaa hiyo itasaidia sana katika maeneo yenye shida ya maji, hivyo atawasiliana na wilaya za pembezoni ili waisambaze kwa wananchi kwa kuwa uhitaji ni mkubwa sana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Super Brand  Ltd Bwana David Mulokozi amesema wameamua kutengeneza Vitakamkasa mikono ili kuwasaidia wananchi waweze kujikinga na virus vya covid 19 kwa kuwauzia kwa bei ambayo mwananchi wa kawaida anaweza kumudu kununua kwani wanauza kuanzia  Shilingi 1500 Mil 50, shilingi 2500 Mil 100, Lita tatu ni Shilingi 75000 na Lita tano ni shilingi 125000.

Kiwanda cha Mati Super Brand Ltd  kinachojihusisha na utengezaji wa Vinywaji vikali kimeanza kutengeneza vitakasa mikono mara baada ya kufumuka kwa ugonjwa wa Corona na nchi kuingia kwenye uhitaji mkubwa wa Vitakasa mikono

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.