• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Mnyeti azipongeza Halmashauri za Manyara kwa kupata hati safi

Imechapishwa Tarehe: May 29th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa  Manyara Mhe.Alexander Mnyeti amezipongeza Halmashauri zote saba za Mkoa wa Manyara kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo kwa miaka ya fedha ya  2016/17,2017/18 na 2018/19 kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Mnyeti alitoa pongezi hizo akiwa katika ziara ya kutembelea Mabaraza ya Madiwani ya kupitia hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali yaliyofanyika katika makao Makuu ya Halmashauri hizo kuanzia tarehe 28 hadi 29 mwezi Mei.

“Kwa kweli lazima niwapongeze Madiwani na Wataalam wote katika kila Halmashauri ya Mkoa wa Manyara kwa kuhakikisha tunapata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo kwani miaka ya nyuma hali haikuwa kama ilivyo sasa,hongereni sana”Alisema Mkuu wa Mkoa.

Pamoja na pongezi hizo pia alimtaka Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali kuhakikisha baadhi ya hoja kama za upungufu wa watumishi na kupewa ukuu wa Idara/kitengo zinaondolewa kwa Halmashauri kwa kuwa hizo ni hoja za kisera na kamwe hazihusiani na Madiwani kwani Madiwani hawana uwezo wa kutatua tatizo la upungufu katika Halmashauri.

“Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali kuna baadhi ya hoja kwa kweli ni vema mkawakague Wizara ya Utumishi na TAMISEMI ndo muwaulize kwanini hawaleti watumishi na kuwapandisha vyeo watumishi waliokaimu Idara/Vitengo kwa muda mrefu Mkoa wa Manyara” Alisisitiza Mheshimiwa Mnyeti.

Akijibu hoja hiyo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali  Mkoa wa Manyara Bwana Paschal Mawago alisema kuwa watajitahidi kukaa na wataalam wa Halmashauri kuhakikisha kuwa hoja zote za kisera zinafutwa na pia aliwataka wataalam kufika katika Ofisi za Mkaguzi zilizopo Babati wakati wowote wapatapo vielelezo vya baadhi ya hoja ili kuzifuta na kuzifunga.

Akiwa katika Baraza la Madiwani Wilayani Kiteto Mkuu wa Mkoa pia alishuhudia Diwani wa viti Maalum Mheshimiwa Zamda  kutoka CHADEMA alitumia nafasi hiyo kukihama chama chake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Mheshimiwa Mwenyekiti kuanzia leo tarehe 28 Mei mimi nikiwa kama Diwani wa CHADEMA nimeamua kujiunga na CCM bila kushawishiwa na mtu yoyote kwani sioni jambo la maana watakalofanya CHADEMA ambalo Mheshimiwa Rais  John Pombe Magufuli hajafanya.Alisema Mheshimiwa Zamda.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa pia alitumia ziara hiyo kuwaaga na kuwatakia kila la heri  Madiwani na Wabunge wote wa Mkoa wa Manyara kwani Mabaraza yote ya Madiwani yanatarajiwa kuvunjwa kuanzia tarehe 10  Juni 2020 ili kupisha mchakato uchaguzi Mkuu wa Madiwani,Wabunge na Rais kuanza na pia kuwataka Wakuu wa Idara kusimamia vizuri Halmashauri katika kipindi hicho ambacho Halmashauri hazitakuwa na Mabaraza ya Madiwani.

“Kwa kuwa hili ni Baraza la mwisho kabla ya Baraza kuvunjwa nitumie nafasi hii kuwatakia kila la heri Mdiwani katika uchaguzi ujao wa mwezi Oktoba, naamini asilimia zaidi ya tisini mtarudi baada ya uchaguzi na pia katika kipindi hiki nawataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara kuhakikisha mnadhibibiti matumizi ya fedha” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

(Kwa picha mbalimbali  angalia sehemu ya  Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha)

Imeandikwa na:Haji A.Msovu

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.