• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

RC Sendiga aridhishwa na Miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru 2023

Imechapishwa Tarehe: October 2nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi itakayo zinduliwa na kutembelewa na Mwenge wa Uhuru 2023 katika Halmashauri ya Mji wa Babati na Halmashauri ya Babati Wilaya. Katika ziara hiyo, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameambatana na Katibu Tawala Mkoa Bi. Karolina Mthapula,  kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange.

Mhe. Sendiga mefanya ukaguzi wa eneo lakupokea Mwenge Uhuru 2023 lililopo kijiji cha kiongozi Kata ya Maisaka katika Halmashauri ya Mji wa Babati ambapo amewataka viongozi kutoa hamasa ilikufanikisha mapokezi ya Mwenge katika eneo hilo. Pia ametembelea mradi wa maji unaosimamiwa na kutekelezwa na Wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA) katika mtaa wa Maisaka Kati Kata ya Maisaka ambapo ametoa maelekezo kuhusu mradi huo na kusisitiza usafi.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea mradi wa utunzaji mazingira uliyopo mtaa wa Maisaka Kati Kata ya Maisaka sambamba na hilo amefanya ukaguzi wa Klabu za kupinga Rushwa  katika shule ya Sekondari Kwaraa iliyopo katika Kata ya Babati. Nao wanafunzi wa Klabu hiyo katika shule ya Kwaraa, wameonyesha igizo fupi kuhusu upingaji wa rushwa, aidha Mhe. RC amesisitiza  juu ya utunzaji wa mazingira katika shule hiyo.

Pia amefanya ukaguzi wa mradi wa karavati katika kijiji cha Mutuka Kata ya Mutuka na kutoa maelekezo kuhusu mradi huo. Vilevile amefanya ukaguzi wa mradi wa madarasa matatu katika shule ya msingi Hangoni iliyopo Kata ya Babati zote zikiwa katika Halmashauri ya Mji wa Babati. Mhe. Mkuu wa Mkoa amewapongeza kwa kutekeleza mradi huo vizuri huku akiwataka kukamilisha miradi yote kwa wakati.

Aidha, Mhe. Sendiga amefanya ukaguzi wa Daraja la Bacho lililopo Kata ya Ayalagaya Kijiji cha Haysam katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati. Pia, amefanya ukaguzi katika shule ya msingi Masabeda iliyopo Kata ya Bashinet Kijiji cha Masabeda. Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake na kufanya ukaguzi wa mradi wa maji uliokuwa ukitekelezwa na RUWASA katika Kata ya Nar kijiji cha Nar ambapo amefurahishwa na mradi huo utakao ondoa tatizo la maji katika kijiji hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.