• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

RC SENDIGA AWATAKA WAMILIKI WA MIGODI SIMANJIRO KUJIKITA KATIKA KUPUNGUZA UGONJWA WA TB NA SILICOSIS

Imechapishwa Tarehe: October 20th, 2025

Na, Ruth Kyelula, Manyara RS

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amewataka wamiliki wa migodi ya Tanzanite, Mirerani Wilayani Simanjiro, wajikite katika kupunguza ongezeko la ugonjwa wa TB na Silicosis kwa wachimbaji wao kutokana na vumbi la madini kuathiri mapafu ya wachimbaji, wawapo katika zoezi la uchimbaji madini kama ivyoainishwa kwenye utafiti uliofwanywa na mtafiti kutoka chuo kikuu Ardhi, Dar-es-Salaam (Dr. Manti M. Nota) kwa kushirikiana na Gem Legacy.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe.Queen Sendiga, akizungumza na Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Muhaji, katika kikao cha wamiliki wa migodi ya Tanzanite, Simanjiro.


Aliyasema hayo wakati wa kikao chake na wamiliki wa migodi ya Tanzanite pamoja na wataalamu mbalimbali wa ngazi ya Mkoa na Wilaya, kilichofanyika katika ukumbi wa Mazubu Grand Hotel, katika mji mdogo wa Mirerani,Wilayani Simanjiro, Oktoba 20, 2025.

Baadhi ya wamiliki wa migodi ya Tanzanite, Wilayani Simanjiro, wakifuatilia kikao cha mhe. RC.

"Niwaombe wamiliki wa migodi muweze kuchimba visima vya maji ama muweke ma tanki kwenye migodi yenu, ili mkiwa kwenye shughuli zenu za uchimbaji mmwagie maji kama wataalamu walivyoshauri kwenye utafiti ili kupunguza vumbi jingi linaloingia kwenye mapafu na kupelekea TB na Silicosis kwa wachimbaji badala yake tuchimbe na maji ili kulinda afya zetu na wafanyakazi wetu." Alisema Sendiga.

Aidha amewataka wamiliki wa migodi hiyo, kuhakikisha usalama wa afya za wachimbaji wao wa madini, pamoja na kuwapa elimu namna ya kujikinga dhidi ya magonjwa hayo lakini pia wawe na utaratibu wa ucheki afya zao mara kwa mara ili pia waweze kupata matibabu mapema.


Kwa upande mwingine Mhe.Sendiga amewaasa wamiliki hao wa migodi kufanya (CSR) kurudisha sehemu ya wanachopa kwa jamii,ili jamii nayo inufaike na uwepo wa migodi hiyo katika maeneo wanayoishi. Na aliwashukuru kwa mwaka jana kuweza kutoa CSR ya milioni arobaini (40) kwa jamii.


Mwisho Mhe. Sendiga aliwakumbusha na kutoa wito kwa wamiliki hao wa migodi ya Tanzanite, kushiriki uchaguzi mkuu, ifikapo Oktoba 29, 2025, watumie haki yao ya kikatiba waende kwenye vituo vya kupigia kura na wapige kura kwa Amani na utulivu.           

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                           

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • MKUU WA MKOA WA MANYARA ATETA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSIANA NA UCHAGUZI MKUU 2025

    October 21, 2025
  • RC SENDIGA AWATAKA WAMILIKI WA MIGODI SIMANJIRO KUJIKITA KATIKA KUPUNGUZA UGONJWA WA TB NA SILICOSIS

    October 20, 2025
  • WAJASIRIAMALI MKOA WA MANYARA WATAKIWA KUONGEZEA THAMANI MAZAO YA MBOGAMBOGA NA MIKUNDE

    October 10, 2025
  • RAS MANYARA ASAPOTI MPANGO WA SHIRIKA LA EGPAF IFIKAPO 2028 ASIZALIWE MTOTO MWENYE HIV

    September 22, 2025
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.