• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

RUWASA pelekeni maji mashuleni - Katibu Tawala Manyara

Imechapishwa Tarehe: May 13th, 2020

Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bwana Missaile Musa ameitaka Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (Rural Water Supply and Sanitation Agency –RUWASA) Mkoa wa Manyara kuhakikisha huduma za maji zinafika katika maeneo mengi Mkoani Manyara ikiwemo katika maeneo ya Shule,Zahanati na Vituo vya afya kwani sehemu hizo ni muhimu kuwa na huduma ya maji muda wote.

Katibu Tawala ameyasema hayo leo Jumatano wakati wa kikao cha Kamati ya Lishe  Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa jingo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara mara baada ya Kaimu Meneja wa RUWASA mkoa Mhandisi  Wolta Kirita aliposoma taarifa ya hali ya upatikanaji wa maji Mkoani Manyara. Kaimu Meneja huyo alisema hali ya upatikanaji wa maji ni kwani mpaka sasa upatikanaji wa maji Vijijini ni asilimia 55, miji midogo upatikanaji ni asilimia 65 na pia Mamlaka ya Maji Babati BAWASA imeongeza eneo la kutoa huduma ya maji katika miji ya Galapo,Dareda,Bashneti na Mbulu hivyo kufanya sehemu kubwa ya Mkoa wa Manyara kuwa na vyanzo vya uhakika vya maji.

Akizungumzia changamoto za usalama wa maji yanayopatikana Mtaa wa Mrara na Bonga Kaimu Meneja wa RUWASA alisema kwa sasa wameshaanza kuchukua hatua za kufunga chujio kwa ajili ya kuchuja maji pamoja na kuweka mlinzi ili kusitokee uharibifu wa vyanzo vya maji.

“Tumeanza kuweka chujio la kuchuja maji katika chanzo cha maji Bonga,tukimaliza Bonga tutaweka Mrara ili kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama” Aliseme Mhandisi Kirita.

Akizungumzia juu ya Miradi ya Maji Mkoani Manyara Kaimu huyo wa RUWASA alisema RUWASA itahakikisha Wilaya zote za Mkoa wa Manyara zinapata maji ya uhakika na kwa kwa sasa kuna miradi ya Olchoronyori,Olbili Wilayani Simanjiro,Malangi katika Wilaya ya Babati na mradi mkubwa wa maji unatarijiwa kujengwa katika wilaya ya Kiteto utakaohudumia wilaya ya Kiteto na Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bwana Missaile Musa alisifu kazi zinazofanywa na RUWASA Mkoa kwa kuhakikisha huduma za maji zinapatikana kwa uhakika.

“Kwa kweli pamoja na ugeni wako Mhandisi wa Maji lakini umejitahidi kuhakikisha umetembelea maeneo yote yenye changamoto za maji na kuzitatu” Alisema Katibu Tawala.

Akisoma Taarifa ya Lishe Moa Afisa lishe Mkoa wa Manyara Bwana Mabula Migata alisema ugawaji wa chakula kwa shule za Sekondari ni asilimia mia moja kwani shule zote 151 za serikali zilizopo mkoani Manyara zinagawa chakula kwa wanafunzi na kwa upande wa shule za msingi ugawaji wa chakula ni asilimia 80 ya shule zote za serikali zinazogawa chakula kati ya shule 603 za msingi zilizopo mkoani Manyara.  

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • RC Manyara amaliza Mgogoro wa ardhi baina ya mwekezaji na wananchi

    September 01, 2021
  • Mkirikiti amkabidhi Makongoro Ofisi rasmi

    May 25, 2021
  • Karibu Manyara Mhe. Makongoro Nyerere!!!

    May 22, 2021
  • Tuweke uzalendo ktk kusajili watoto chini ya miaka mitano - RC Manyara

    April 20, 2021
  • Tazama Zote

Video

Asilimia mbili ya mikopo kwa walemavu
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2021 Manyara Region . All rights reserved.