• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Serikali Yatenga Bilioni 29.9 Kumalizia Maboma Yote ya Shule

Imechapishwa Tarehe: February 19th, 2019

Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 29.9 kwa ajili ya kumalizia maboma yapatayo 2,392 nchini kote ili kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu wanaanza masomo mara moja kabla ya kumalizika mwezi machi, 2019.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga katika Manispaa ya Musoma jana wakati akiongea na watumishi wa ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Kamati tendaji za Halmashauri ya Manispaa Musoma na Halmashauri ya wilaya Musoma baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi katika halmashauri hizo hii leo.

“katika kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza na hawakupata nafasi hapa nchini mwaka 2019, Serikali ya Daktari John Pombe Joseph Magufuli imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 29.9 ili kujenga maboma 2,392 ambapo wataweza kuendelea na masomo yao” alisema Nyamhanga.

Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa wanafunzi wapatao 133,737 hawakupata nafasi kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu wa 2019 na ndio Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameamua kutolewa kwa fedha hizo kumaliza tatizo hilo.

Nyamhanga amesisitiza watendaji wote wa mikoa kusimamia fedha hizo na kwamba tayari zimeingizwa katika akaunti za shule husika zenye maboma na hivyo ukamilishaji wa maboma hayo ni lazima uwe wa muda mfupi ili wanafunzi waanze kuanza masomo yao mapema iwezekanavyo. Amesema maboma hayo lazima yakamilike kabla ya kumalizika mwezi machi, 2019 kama ilivyopangwa.

“Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa shule, Bodi za shule na kamati lazima zisimamie fedha hizo, mimi na ofisi yangu tutapita shule hadi shule na kuhakikisha kama fedha zilizopelekwa zimetuka kwa malengo yaliyokusudiwa” alisema Nyamhanga.

Imeandikwa Na: Fred Kibano

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.