• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Wafanyabiashara Manyara waunganishwa na Indonesia

Imechapishwa Tarehe: December 10th, 2019

Balozi wa Indonesia nchini Tanzania amewaahidi  wafanyabiashara Mkoani manyara  kuwaunganisha na wafanyabiashara  wa nchi ya Indonesia ili waweze kufanya  biashara kwa  pamoja  na kuendelea kujenga mahusiano kati ya nchi ya Tanzania na Indonesia.

Akizungumza katika mkutano  na wafanyabiashara  wa  mkoani Manyara jana katika  ziara yake  ya kuangalia fursa za  biashara na uwekezaji yenye nia ya kuboresha uhusiano wa nchi hizo  kiuchumi alisema wafanyabiashara wanafursa nzuri ya kufanya biashara na nchi ya Indonesia kwani nchi hiyo ni miongoni mwa nchi zilizoendelea huku zikiwa na fursa nyingi ikiwa na kutengeneza mashine mbalimbali za uchakata   nafaka na zana za kilimo.

Balozi  huyo alisema kwa sasa biashara inayofanywa kutoka Indonesia kuja Tanzania  haifiki kwa  walengwa moja kwa moja na badala yake kumekuwa  na walanguzi  ambao wanaziongeza gharama na kuziuza bidhaa hizo kwa wafanyabiashara  jambo ambalo kwa sasa anataka kuliondoa kwa kuwaunganisha wafanyabiashara moja kwa moja kutoka Indonesia.

“Kwa Sasa ni Bidhaa hamsini tu za Indonesia zianazoletwa Tanzania ambazo ni mafuta ya mawese, Makaratasi,   Tanzania  inapeleka Tumbaku, Pamba,Karafuu na Mwani’’

“Serikali ya sasa inataka kutumia mahusiano ya kisiasa kuwa ya kiuchumi  ili kuifanya Tanzania kuwa chi ya viwanda na uchumi wa kati hivyo ziara yangu itasababisha uhusiano mzuri kati ya wanfanyabiashara

wa Manyara na Mkoa mmoja wa Indonesia , ntatembelea mikoa yote 31 kuangalia fursa mbali mbali na huu ni mkoa wangu wa 13” alisema.

Naye Afisa wa Wizara ya Mambo ya nje  Rwangisa Francis  alisema kuwa kuwa balozi huyo amefika mkoani hapo kwaajili yabuwekezaji wa viwanda na biashara na hatua hiyo iimekuja mara baada ya balozi huyo alipokuwa

akiwasiliosha hati zake za utambulisho mwaka 2017  kwa Rais  wa Jamhuri ya muunganno wa Tanzania Dkt John P. Magufuli na kumuahudi kuwa kwa kuwa Tanzania ni nchi ya viwanda  na wao Indonesia wataisaidia kuwa nchi ya viwanda.

“Mikoa ya Tanzania  31 na Indonesia kuna mikoa 34 sasa anapokuja katika mkoa flani anaangalia fursa  mbali mbali za  zinazojitokeza  za uwekezaji na biashara  akishaziona anakwenda kule kwao anazungumza na wahusika  na kuangalia mikoa  inayolingana kifursa na kuiunganisha ili waweze kufanya biashara na kuzalisha’’ alisema  Francis.

Alisema kufuatia ziara hiyo anatarajia kama zoezi hilo litafanikiwa atawaleta wawekezaji watakaowekeza kwa makubaliano au wawekezaji wa moja kwa moja ili watanzania waweze kufanya biashara , ikiwa ni pamoja na kuongezeka idadi ya viwanda na ajira.

Kwa upande wake katibu wa Chama cha Wafanyabiashara  Mkoani  humo TCCIA  Mwanahamisi Husen alisema ujio wa balozi huyo mkoani hapo umeleta matumaini kwani  balozi huyo ameahidi kuunganisha TCCIA  ya Mkoani manyara na ya  mkoa mmoja wa Indonesia ili waweze kufanya kazi kwa pamoja na kuwatafutia wafanyabiashara  fursa mbali mbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.