• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

WASIOENDELEZA VIWANJA BABATI KUNYANG'ANYWA

Imechapishwa Tarehe: June 27th, 2019

MKUU wa mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti ameitaka Idara ya Ardhi ya halmashauri ya mji wa Babati mkoani hapa kunyang'anya viwanja vyote vilivyoshindikana kuendelezwa ndani ya miaka mitatu.

Mnyeti aliyasema hayo jana katika kikao cha Baraza la Madiwani la kujibu hoja za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) ambapo halmshauri hiyo imepata hati safi.

Mnyeti alisema wale wote wanaodaiwa hela ya viwanja na wameshindwa kuvilipia ndani ya miaka mitatu ikiwa ni pamoja na kushindwa kuviendeleza wanatakiwa wanyang'anywe na kuuziwa watu wengine wenye uhitaji wa viwanja.

"Sasa tukubaliane kwamba wale wote wanaodaiwa kutokana na mauzo ya viwanja wanyang'anywe na wauziwe watu wengine wenye uwezo wa kulipa vinginevyo hii hoja  mwakani isijirudie.

"Kwa taarifa nilizonazo hivi viwanja vingi mmevinunua ninyi na hamtaki kulipa, Ofisa Ardhi pitia majina yote ya watu wanaodaiwa waite waambie mnalipia au hamlipii, na kama hamlipii chukua viwanja vyote tangaza watu wanunue na weka muda fulani hujalipa, kiwanja kinauzwa", Alisema Mnyeti.

Naye Diwani wa viti maalumu Praxidia Claud (Chadema) alimuomba Mnyeti kuingilia kati suala hilo kwani wao kama madiwani wanateseka na jambo hilo hali inayopelekea kulalamika kwamba halmashauri inakosa mapato.

“Mkuu wa mkoa hili ni jipu ambalo linatutesa sana katika halmshauri yetu, mara nyingi tumekuwa tukilalamika sana kwamba halmashauri yetu inakosa mapato, tunashindwa kuwalipa walinzi, tunashindwa kulipa maji, umeme.

“Haiwezekani toka viwanja vimetangazwa mtu kachukua zaidi ya miaka mitatu hajalipia na sisi tunashida na hela hatuna hata pesa ya kuwalipa vibarua wanaotufanyia usafi, kwa dhamira ya dhati Mh.mkuu wa mkoa tunaomba ushikilie hili”, Alisema Claud.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmshauri ya mji wa Babati, Yona Wawo (CCM) alisema toka mwaka 2014 walijiwekea malengo ya kupata fedha nyingi si chini ya Bil. 10 kutokana na mauzo ya viwanja.

“Sasa sababu zilizojitokeza ninatambua kwamba idara yetu ya upande wa ardhi haikufanya vizuri sana watu amepewa viwanja na wengine wana viwanja vingi sana na walichukua kienyeji hawajaweza kuvilipia vyote na imechukua muda wa miaka minne au mitano na hatupati fedha kwa halmashauri.

“Mimi kama Mwenyekiti wa halmashauri kwa sasa, nitahakikisha kwamba viwanja vyote ambavyo havijalipiwa tunavichukua kwa halmashauri tayari tunatangaza upya na tunaweka bei inayoendana na wakati”, Alisema Wawo.

(Kwa picha mbalimbali  angalia sehemu ya  Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha)

Imeandikwa na:Haji A.Msovu


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.