• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

WAZAZI PELEKENI WATOTO VETA-MKUU WA WILAYA YA BABATI

Imechapishwa Tarehe: October 29th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Babati Mheshimiwa Elizabeth Kitundu amewataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliofaulu darasa la saba wanaendelea na elimu ya Sekondari huku kidato cha nne ambao hawatafanikiwa kuendelea kidato cha tano wakiendelea kupata mafunzo katika vyuo vya Ufundi stadi (VETA).

Mkuu wilaya ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na wanafunzi,walimu na wazazi katika mahafali ya 10 kwa shule ya Msingi Rift Valley Babati na ya 5 kwa upande wa Sekondari Rift Valley Babati ambapo amesema baada ya matokeo mwanafunzi akiwa hajapata alama za kumwezesha kuendelea na kidato cha tano asikate tamaa kwani kuna vyuo vya ufundi stadi ambavyo vinatoa mafunzo mbalimbali yatakayowasaidia katika maisha yao.

Mkuu wa wilaya  akawatia moyo  walimu kuongeza bidii katika kufundisha na kuzingatia maadili mema  huku akiwasihi wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao.

Mkurugenzi wa taasisi za Rift  Valley shule ya msingi The Moshi Academy, Northern Highlands Secondary School (NHSS),North Highlands Teachers Training College Henry Stansalaus  Mallya,amesema katika taasisi zake walimu watakaobainika wanakwenda kinyume na maadili wanachukuliwa hatua mbalimbali ikiwemo kuachishwa kazi.

Mkuu wa shule ya Rift Valley Babati Sekondari  Daddly Wilfredy amesema shule hiyo ilianza mwaka 2003 na kupokelewa  rasmi na mmiliki wa sasa mwaka 2012 baada ya waanzilishi kushindwa kuiendesha huku ikiwa na mafanikio makubwa katika taaluma kwa kufaulisha wanafunzi katika madaraja ya juu ambapo wengi wao wamekuwa wakichaguliwa kujiunga katika shule za Sekondari.

Mwalimu mkuu Dadly  amesema mahafali hayo ni ya tano kwa Sekondari huku kukiwa na mafanikio makubwa,ambapo kwa jitihada za walimu wazoefu walionao,shule imekuwa ikifanya vizuri Kimkoa na Kiwilaya nfasi ya tatu nay a nne kila mwaka.

“Kwa kweli tuna kamati ya kuchuja sana watumishi,akitokea mmoja kwa bahati mbaya akafanya tabia zisizofaa hata kama hatuna  uthibitisho,tunamchukulia hatua za papo kwa papo”.alisema Mallya.

Imeandikwa Na: John Walter

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.