• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Waziri Ndalichako awahimiza wananchi wa Mkoa wa Manyara kujitokeza siku ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Oktoba 14

Imechapishwa Tarehe: October 2nd, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Viijana, Kazi, Ajira na watu wenye ulemavu Mhe. Profesa Joyce Ndalichako amefanya ziara ya ukaguzi wa maandalizi ya kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 kitakachofanyika Mkoani Manyara Oktoba 14.

Katika ziara hiyo, Mhe. Ndalichako amepokea taarifa ya maandalizi kwa ujumla kutoka kwa mratibu wa Mbio za Mwenge Mkoa Bw. Samwel Pastory katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Bw. Pastory ameeleza juu ya ukamilishaji wa uwanja wa Kwaraa na amemuhakikishia Waziri Ndalichako kuwa  kamati zote zilizopangwa  zimejipanga vizuri, pia ameeleza kuwa mafunzo kwa upande wa Watoto wa halaiki  yanaendelea na sale za watoto hao zimesha wasili.

Aidha mratibu huyo amemueleza Mhe. Waziri kuwa uhamasishaji unaendelea kwa Halmashauri zote ikiwa ni pamoja na kuandaa bonanza kwaajili ya uhamasishaji mkubwa wa watu kujitokeza kwa wingi.

Vilevile Mhe. Ndalichako ametembelea uwanja wa kwaraa kuona mwenendo wa ujenzi unaoendelea katika uwanja huo. Mhe. Waziri amefurahishwa na kasi ya umaliziaji wa uwanja ikiwa ni pamoja na kuezekwa kwa mapaa katika majukwaa yote matatu, kukamilika kwa eneo la kukimbilia (running track) kwa kiwango cha rami, pia kukamilika kwa nyasi katika eneo la uwanja.

Katika ujio wake, vilevile ametembelea kanisa la Roho Mtakatifu ambako itafanyika Misa maalumu kwaajili ya kumbukizi ya Baba wa Taifa  Hayati Julius Kambarage Nyerere na amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Manyara kwa ujumla kujitokeza siku ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Oktoba 14.

Aidha, Profesa Ndalichako amefanya ukaguzi katika eneo la uwanja wa Stendi ya zamani kutakapo fanyika maonesho ya wiki ya vijana kitaifa, ambapo amewataka vijana kujitokeza kwa wingi katika maonesho ya wiki ya vijana ili kuweza kujifunza na kupata ujuzi wa mambo mbalimbali yenye tija katika maisha yao na kuupongeza Mkoa wa Manyara kwa maandalizi  mazuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.