• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

JAFFO AKEMEA UBADHILIFU WILAYANI HANANG

Imechapishwa Tarehe: September 3rd, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mh. Suleiman Jaffo leo tarehe 03/09/2018 amefanya ziara ya kikazi Wilayani Hanang Mkoani Manyara na kufanya mkutano na watumishi wa wilaya hiyo. Akizungumza na watumishi Mh.Jaffo alisema utendaji wa kazi kwa sasa umebadilika tofauti na zamani hivyo watumishi hawapaswi kubweteka na wala kufanya kazi kwa mazoea pia aliwasisitiza wafanyakazi hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii ,wajenge mahusiano mazuri kati ya Idara na Idara ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana.

Aidha aliwasisitiza wakurugenzi wa wilaya kuendelea kuwapima wafanyakazi hao kama wanafanya kazi vizuri na kama ikitokea wakashindwa kutimiza majukumu yao hawanabudi kuwaondoa na pia aliwataka watumishi hao kuacha ubinafsi, upendeleo na ufisadi wa rasilimali za wananchi na mapato ya serikali kwani Halmashauri yoyote haiwezi kuendeshwa bila mapato.

          Vilevile Mh.Waziri alimtaka Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mh. Joseph Mkirikiti kuunda timu ya kufanya uchunguzi juu ya ukusanyaji wa mapato na kuandaa taarifa sahihi juu ya mapato hayo, Mh. Jaffo alisema “hatuwezi kuruhusu fedha ziende kwa watu wachache kwani katika wilaya ya Hanang ukusanyaji wa mapato bado upo chini na miradi ya kimaendeleo bado hairidhishi hii ni kutokana na kukumbatiwa na watu wachache”.

Halikadhalika Mh. Jaffo alitoa onyo kwa viongozi waliochaguliwa, wabunge, madiwani na wenyeviti wa Halmashauri waache kuingilia maslahi ya Halmashauri kwa matumizi yao binafsi.

Akitoa neno la shukrani Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Alexander Mnyeti alisema “Utumishi ni maswala ya kujitolea hivyo watumishi ni jukumu letu kuwatumikia wananchi na kufanya kazi kwa bidii na maendeleo ya taifa pia alisema kikao hicho kimelenga kujenga, kuongoza na kuelimisha utendaji wa kazi za watumishi pia yale yote yaliyoelekezwa na Mheshimiwa Waziri tuyafanyie kazi na pia ni wajibu wetu kutumia sheria, kanuni na taratibu pia hekima na busara katika kuongoza wananchi.

(Kwa Picha mbalimbali na video angalia Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha na Maktaba ya Video)

Imeandikwa na Isabela Joseph (UDSM-Mafunzo kwa Vitendo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.