• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Wadau Njooni na mpango wa kuendeleza michezo- Naibu Waziri

Imechapishwa Tarehe: April 1st, 2019

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.George Waitara amewataka wadau na wataalamu wa michezo nchini kuja na mpango mahsusi wa namna nchi itakavyoweza kufikia  katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.

Akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kwa ajili ya Mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) kilichoandaliwa na kampuni ya vinywaji ya Coca cola, Mheshimiwa Waitara amesema anatamani kuona walimu na wadau wengine waje na mpango mahsusi wa kuendeleza michezo ili Tanzania iondokane na tabia ya kuwa kichwa cha mwendawazimu katika sekta hiyo.

Mhe.Waitara amesema wataalamu waje na hoja ya kuendeleza sekta na michezo na anaamini kuwa walimu katika hili wana mchango mkubwa katika kuendeleza sekta ya michezo.

Amesema kwa kuwa watanzania wanapenda sana michezo, hakuna sababu ya kuwasononesha na badala yake akataka wataalam wa michezo kuja na mpango kabambe wa kukwamua sekta hiyo.

Mhe.waitara amesema pamoja na mchango mkubwa unaofanywa na walimu nchini katika kuinua maendeleo ya elimu nchini ambapo kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kiwango cha ufaulu kimekuwa kikiongezeka, bado anaamini walimu wana jukumu kubwa katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanafundishwa michezo kwa nadharia na vitendo.

“ Natoa maelekezo kwa walimu wote kuhakikisha kuwa somo la michezo linafundishwa kwa nadharia na vitendo kama mtaala wa elimu unavyoelekeza,” amesema na kuongeza:

“ viwanja vya michezo vifufuliwe na vifanye kazi kama ilivyokusudiwa, viwanja vilivyovamiwa vipimwe na kuwekewa mipaka,” amesema.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya michezo ya umiseta na udhamini kutoka kampuni ya Coca cola, Naibu Waziri ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kudhamini mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika kitaifa mkoani Mtwara kuanzia mwezi juni mwaka huu.

Pia Mhe.Waitara ameipongeza coca cola kwa kuanzisha shindano maalum la kutafuta shule bora zinazoongoza kwa kutunza na kuhifadhi mazingira ambapo mtoto ambaye atafanikiwa kuokota chupa kilo 600 na kuendelea watapata zawadi mbalimbali zikiwemo laptop.

Naibu Waziri amewataka Coca cola kuhakikisha kuwa shindano hilo linazifikia shule nyingi iwezekanavyo na ikibidi lifanyike kwa mikoa yote 26 nchini.

Mhe.Waitara amewaagiza Maafisa Elimu wa Mikoa, na Maafisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazotolewa na kampuni hiyo zinagawiwa kwa walimu watakaoshinda na wanafunzi pia.

Wakati huo huo Naibu Waziri Waitara amewataka Maafisa elimu nchini kuhakikisha kuwa wanawasimamia walimu na wanafunzi ili waweze kupanda miti ya kutosha nchini ili waweze kukabiliana na athari za jangwa.

“Tukitaka kusaidia kampeni ya usafi wa mazingira hatuna budi kuanza na walimu na wanafunzi, tuhakikishe kila mwalimu shuleni anapanda mti mmoja na kila mwanafunzi anapanda miti miwili mmoja nyumbani na mwingine shuleni,” amesema.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Julius Nestory ameipongeza kampuni ya vinywaji ya Coca cola kwa kuendelea kudhamini mashindano ya UMISSETA ambapo mwaka huu kampuni hiyo imeongeza kipengele cha usafi wa mazingira.

Amewataka maafisa elimu kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazonunuliwa na wadhamini coca cola zinawafikia walengwa na kwamba zawadi na jezi hizo kamwe zisiishie mitaani kwa wasiohusika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.