• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

WAZAZI WAONYWA KUTOOZESHA WATOTO

Imechapishwa Tarehe: June 16th, 2019

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa Mzee  Mkongea Alli amewataka wazazi kuacha tabia ya kuwaozesha watoto wa kike mapema, kwani kitendo hiko  kinawanyima fursa nyingi za maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuzindua mradi wa madarasa 8 na ofisi 3 katika Shule ya msingi Bacho  kata ya Dareda halmashauri ya wilaya ya Babari, alisema  kitendo chabkumuozesha mtoto wa kike mapema ni kumnyika haki yake ya msingi.

Alisema wazazi wana jukumu la kuhakikisha  anamsimamia kikamilifu mtoto wake wa kike ili kuweza kumsaidia kutimiza wajibu wake ili kutimiza nankufikisha ndoto za mtoto katika kuhakikisha anatimiza malengo yake ya kusoma kikamilifu, na si vingine.

" Wazazi wenzangu tuache tabia ya kuwaozesha mapema watoto wetu, hili ni tatizo kubwa sana ambalo litawanyima  fursa watoto wa kike kutokusoma, unapomuozesha mtoto wa kike mapema bila ridhaa yake unamvunjia fursa nyingi sana za maendeleo , unamsababaishia maambukizi ya VVU Ukimwi, unamsukumiza kwa mtu ambaye hana interest naye, hamuelewi, lakini pia kunapelekea vifo vya mama na mtoto" alisema Mkongea Ali

Aidha aliwataka walimu kutunza miundombinu hiyo kwani wahisani walijitokeza kujenga miundombinu hiyo kwakua waliona utendaji wao wa mzuri wa  kazi, hivyo wametakiwa  kuhakikisha wanatunza miundombinu hiyo ili wahisani wapate moyo wa kutoa zaidi ya walichotoa kwani wametumia pesa nyingi kukamilisha Ujenzi wa Mardi.

Aidha aliwapongeza wahisani waliojenga mradi huo pamoja na wananchi kwa kuchangia nguvu kazi zao kwa kuhakikisha wanawawekea miundombinu  mizuri ya elimu ili watoto waweze kusoma katika miundombinu mizuri.

" Niwashukuru wananchi kwa nguvu zenu ni kazi Nzuri sana ambayo tumeiona, lakini pia niwashukuru wafadhili wetu ambao wamefadhili kwa kiasi kikubwa sana kuhakikisha wanatuletea miundombinu mizuri ya elimu ili watoto wetu wapate wlimu bora,  hivyo wananchi nadhani mmejionea miundombinu mizuri sana inavutia yaani unapoingia darasani unatamani mwalimu awepo afundiishe" alisema

Aidha aliwageukia wanafunzi kuhakikisha wanajijengea mazingira ya kupenda kusoma ili kuweza kutimiza ndoto zao, kwani hatma ya maisha yako iko mikononi mwao, hivyo wana kila sababu ya kuhakikisha kuwa wanasoma kwa bidii ili kuwatia moyo wazazi wanaowasomesha.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Babati mkoani Manyara Elizabert Kitundu wakati wa makabidhiano  ya mwenge wa uhuru kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga alisema jumla ya miradi 7 yenye thamani ya zaidi ya mil.600,ambayo imetembelewa, kuzinduliwa, kuwekewa jiwe la msingi katika halmashauri hiyo.

Aidha Kitundu  alifafanua kuwa Mwenge wa Uhuru ulikimbiza kwa umbali wa km. 150, huku wananchi wakichangia sh .mil. 96.8 , halmashauri wamechangia sh.mil. 8.6, serikali kuu imechangia sh.mil. 370.9 huku wahisani wakiwa wamechangia sh.mil.167.1

Hata hivyo Kiongozi huyo alimtaka mkuu wa wilaya huyo kuhakikisha anaendelea kuifuatilia miradi mbalimbali inayoendelwa katika wilaya yake.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo aliupongeza uongozi wa Shule ya sekondari kwa kuwafundisha wanafunzi nyimbo nzuri ya uchaguzi wa serikali za mitaa, kufuatia wimbo huo amemtaka mkuu wa wilaya hiyo Elizabert Kitundu kuhakikisha anaufuatilia wimbo na kuhakikisha unarekodiwa ili ifikapo siku ya uchaguzi wimbo huo uweze kutumika.

(Kwa picha mbalimbali  angalia sehemu ya  Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha)

Imeandikwa na:Haji A.Msovu


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.