• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

MANYARA WAZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU

Imechapishwa Tarehe: August 30th, 2018

Kampeni za upimaji virusi vya ukimwi kwa hiari zilizinduliwa rasmi tarehe 29/8/2018 katika wilaya ya Hanang mkoa wa  Manyara. Kampeni hizo zililenga kuhamasisha, kuelimisha na juu ya upimaji wa VVU/UKIMWI, uzaziwa mpango na kifua kikuu na pia kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za ili kufikia malengo ya kitaifa 90, 90, 90 ifikapo mwaka 2030.

(Baadhi ya wadau waliojitokeza katika kampeni ya Furaha Yangu-Pima,Jitambue, Ishi iliyozinduliwa kimkoa Wilayani Hanang 29 Augusti,2018.)

Akisoma taarifa ya mradi wa Taasisi inayoongozwa na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mh.Benjamin Mkapa (Benjamin Mkapa Foundation) Dkt Daud  Isaya alisema taasisi yao inatekeleza mradi wa upimaji jumuishi wa VVU/UKIMWI na kifua kikuu na kuwaelimisha wananchi juu ya tabia hatarishi ziletazo maambukizi ya virusi na kuwahamisha wawe na tabia za kupima afya zao mara kwa mara. Taasisi yetu inatekeleza mradi huu kwa muda wa miaka 3 ambao umeanza  June2018 hadi Disemba 2020,katika utekelezaji kwa Mkoa wa Manyara umeanza June katika Halmashauri mbili ambazo ni Simanjiro na Mbulu.

Katika Wilaya ya Hanang mradi huu ulianza tarehe 25 agosti na mpaka kufikia tarehe 28 mwezi huu jumla ya watu 1826 walijitokeza kupata huduma mbalimbali za kiafya kati yao wanaume 771 na wanawake  655 walipimwa  kati yao watu 5 waligundulika kuwa na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi ambapo  3 ni wanaume na wa 2 ni wanawake wote waliunganishwa na huduma za matunzo na matibabu kwa vituo vya karibu.


(Baadhi ya wadau waliojitokeza katika kampeni ya Furaha Yangu-Pima,Jitambue, Ishi iliyozinduliwa kimkoa Wilayani Hanang 29 Augusti,2018.)

Vilevile uchunguzi wa awali wa kifua kikuu ulifanyika jumla ya watu 1422,walipimwa katiyao  33 walikutwa na dalili za kifua kikuu na kupewa rufaa kwenda hospitali ya Wilaya, upimaji wa shinikizo la damu jumla ya watu  1084 walipimwa kati yao 32 walikutwa na shinikizo la damu lisilo la kawaida na pia upimaji wa kiwango cha sukari jumla ya watu 102 walipimwa kati yao 7 walikutwa na kiwango cha sukari kisicho  cha kawaida. Zoezi hili pia liliambatana na uchangiaji wa damu salama ambapo jumla ya chupa50 za damu zilikusanywa.

Huduma nyingine zilizotolewa ni uzazi wa mpango ikiwamo ugawaji wa kondomu ambapo jumla ya kondomu 4320 ziligawiwa, aidha elimu za ujasiriamali kutoka katika taasisi za kifedha kama NMB na CRDB zilikuwepo, elimu za mienendo ya tabia kupitia vikundi vya ngoma na sinema pia zilitolewa.

Aidha napenda kuishukuru serikali ya Tanzania na ya Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na taasisi yetu katika mradi huu na miradi mingine mingi iliyoanzishwa kwa ajili ya kuimarisha huduma za afya.


(Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mh.Joseph Mkirikiti akisalimiana Mratibu wa Mkapa Foundation Dkt.Daudi Isaya katika kampeni ya Furaha Yangu-Pima,Jitambue, Ishi iliyozinduliwa kimkoa Wilayani Hanang 29 Augusti,2018.)


Akitoa hotuba yake Mgeni rasmi katika sherehe hizo Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mh.Joseph Mkirikiti alisema kuwa “bado idadi ya wanaume katika upimaji hairidhishi hivyo nawasihi waendelee kujitokeza kupima afya zao na pia kwa wanawake wasikate tama waje kupima na wazidi kuwaasa waume zao nao waje kupima afya zao” alisisitiza. Aidha aliwataka wananchi wawe na tabia za kwenda kupima afya zao na ili kufikia malengo ya 90, 90, 90 ni lazima kila mtu apime kwani mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI  yanamhusu kila mtu katika jamii.

 Vilevile alizitaka mamlaka zinazohusika na afya bora kutilia mkazo kampeni za uchimbaji wa Vyoo kupitia kauli mbiu isemayo  “ Usichukulie poa Nyumba ni choo”  ili kufikia malengo ya afya bora ni lazima kila kaya iwe na choo na pia kuhakikisha wanyama kama Mbwa wanafuungiwa kwani idadi yao imezidi kuwa kubwa na wanazagaa mitaani hivyo wanaweza kusababisha madhara kwa wananchi.

(Baadhi ya wadau waliojitokeza katika kampeni ya Furaha Yangu-Pima,Jitambue, Ishi iliyozinduliwa kimkoa Wilayani Hanang 29 Augusti,2018.)

Akimalizia hotuba yake alitoa shukrani kwa mashirika, wadau, taasisi na wananchi waliohudhuria kuifanikisha sherehe hiyo na pia aliishukuru serikali ya awamu ya tano kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi  inavyojikita katika mpango wa maendeleo na kuboresha miundo mbinu na vituo bora  vya Afya, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu  2018 ni “Furaha yangu- pima, jitambue, ishi”.

(Kwa Picha mbalimbali na video angalia Kituo cha Habari kisha nenda Maktaba ya Picha na Maktaba ya Video)

Imeandikwa na Isabela Joseph (UDSM-Mafunzo kwa Vitendo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.